Uingereza imesema pindi tu muungano huo utakapofanya hivyo, basi itatilia maanani swala la kuwatambua rasmi kama muungano halali wa upinzani kwa utawala wa rais Bashar Al Assad. Tayari Ufaransa, Uturuki na mataifa ya eneo la Guba yanautambua rasmi muungano huo wa upinzani.
Wanachama wa muungano mpya wa upinzani, Syria
Kwa upande mwengine Ufaransa imesema itazungumza pamoja na wanachama wengine 27 wa Umoja wa Ulaya juu ya pendekezo la kupunguza vikwazo vya silaha vya Umoja huo ambavyo kwa sasa vinazihusu pande zote mbili zinazohusika na vita vya Syria. Lakini Urusi imesema hatua yoyote ya aina hiyo itakuwa ni kukiuka sheria ya kimataifa .
Jengo moja likiwaka moto nchini Syria
"Hakuna haja ya kuupa sura ya kijeshi mzozo huu. Lakini haikubaliki pia kuona maeneo yaliyokombolewa,yanashambuliwa kwa mabomu. Lazima pawepo wizani,na si rahisi. Kwa upande mmoja kutoingilia upande wa kijeshi na upande wa pili kuzuwia maeneo yaliyokombolewa yasibomolewe. Ndio maana suala la kupelekwa silaha za kujilinda linabidi lizushwe hapa." amesema Laurent Fabius
Umoja wa Mataifa walalamika
Wakati huo huo kwa mujibu wa barua iliyolifikia shirika laahabari la AFP hapo jana Umoja wa mataifa umelalamika kwa serikali ya Syria kwa kudai kwamba ilikuwa na ruhusa ya umoja huo kuwashambulia waasi katika eneo la milima ya Golan ambalo halipaswi kuwa na harakati zozote za kijeshi.
Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia amani Herve Ladsous
Tangu kuanza kwa mapigano nchini Syria miezi 20 iliopita tariban watu 39,000 wameuwawa
No comments:
Post a Comment