..

..
.

MAKALA ZILIZOMO

 KUFIKIA KILELE KWA MWANAMKE KUKO HIV Mambo mengi yanayohusu mwanamke yameandikwa na wanaume.Jambo hili limesababisha kuwepo na taarifa nyingi za kutia mashaka kuhusu mwanamke.Dr Marie Robinson ni mwanamke aliyeolewa.Katika utafiti wake juu ya mwanamke kufika kilele ktk tendo la ndoa anasema hivi Kufika kilele ni ule muda ambao kushikamana kwa msuli na akili huzuka ghafla mpaka kufikia ambapo haiwezekani kwa mwili kuvumilia.

Huku mwanaume akiendelea kusukuma kwa nguvu hali ya raha ya mwanamke huongezeka sambamba na msukumo wa kiuno cha mwanamke. Mwanamke hujikaza kupita kiasi,mpaka pale ambapo huona haiwezekani kuendelea,,maana wakati huo tayari mwili mzima hutikiswa kwa mawimbi ya furaha.

Hapo mwanamke huonekana usoni,mikononi,miguuni,ktk kiwiliwili na ndani kabisa ya nyayo za miguu.

Hayo yote humfanya mwanamke bila kujijua anafanya nini au anatamka nini,kichwa chake hurudishwa nyuma,na sehemu ya chini huinuka juu katika juhudi za yeye kutaka aingiwe zaidi na zaidi.Ikifika hatua hii wanawake hutofautiana,wengine hutumia dk 1,2 au 3

Na habari njema ambayo mwanamke angependa kuisikia ni kumwona mwanaume akiongeza juhudi na juhudi,ili amfikishe zaidi na zaidi ili anapohema kwa nguvu,kusukana kwa mapigo ya moyo na utoaji wa maji ktk tezi vibaki katika hali hii ambayo raha yake ni kufika kileleni kwa pamoja,hakuelezewi kwa maneno bali tabasamu angavu na shangwe za mwili kwa siku nzima inayofuata.

Si wanawake wote hulia au kupiga makelele wengine hujitokeza bila hata wao kujua wanafanya nini,wengine huwa kimya kabisa,wengine hukunja sura zao,wengine huongea lugha wasizozijua,wengine huelemewa na raha kiasi hububujikwa machozi pasipo kutoa sauti,,Lakini dalili kama jasho jembamba,kuhema kwa nguvu,uke kujifinya ili ubane uume,matiti na chuchu kuvimba n.k Ni dalili ambazo huonekana kwa wengi,wanapofikia juu kabisa ya kilele wakati wa tendo la ndoa.

MWANAUME Mjali mwenzako,hakikisha unamsaidia mwenzi wako kupanda mlima huu mrefu kuliko yote duniani.Kutoa mbegu tu na kugeukia upande wako ni ubinafsi!

Fanya kazi kwa moyo,na maarifa Uhusiano utadumu kupita milele

KUMBE VIGEZO HIVI VINAWEZA KUSABABISHA MWANAUME KUKIMBIWA NA WANAWAKE?...!!! SOMA ZAIDI HAPA


1. Wakikosa attention yako. Wasichana hupenda pale wanapofahamu kuwa unawasikiliza na unafahamu nini wao wanahitaji. Kama kutakosekana mawasiliano mazuri na atagundua hilo atauona uhusiano huo haumtimilizii haja zake. Hata kama kila kitu kinaenda sawa. Msikilize anapoongea. Kama akiona hapati penzi analolihitaji atatafuta mwingine ambaye yupo tayari kumtimizia.
2. Kumuheshimu. Msichana huwa anajitoa sana awapo katika mahusiano hivyo anategemea mvulana uheshimu hata kwa chochote kidogo anachokufanyia. Mfanye agundue kuwa umeheshimu kile ambacho amekufanyia.


3. Usaliti. Unaposaliti inamaanisha kuna kitu hakipo sawa katika mahusiano yako hata kama una uwezo wa kushughulikia lakini wewe unaona njia sahihi ni kutoka nje kuwa na mahusiano na msichana mwingine ukidhani ndio unarekebisha. Pale msichana wako akikukamata unamsaliti fahamu hawezi kuvumilia naye atakuacha.


4. Ukosefu wa hisia za kimapenzi. Msichana hupenda kuona kuwa wanapendwa wanathaminwa na wapenzi wao wanawajali sasa wakiona kuwa hakuna conection ya hisia za kimapenzi kutoka kwa mvulana wake huona kuwa hakuna mapenzi ya kweli katika uhusiano aliopo


5. Hawapendi kusikia kuhusu mapenzi mara kwa mara wasichana hupenda kutumia muda mrefu na wapenzi wao bila kusikia neno la kuwataka wafanye mapenzi kama ukiwa nao na ukawataka kimapenzi mara kwa mara watakuwa wanakuavoid hata utakapokuwa ukiwagusa.


6. Unapomcontrol sana
msichana humpenda mvulana atakayemlinda na kujiona yupo sehemu salama sio kumdhibiti kufanya mambo yake mengine anapenda uhuru
......................................................

SINA HAMU NA MWANAMKE TENA HATA AWE MZURI KIASI GANI 


 Najisikia sihitaji mwanamke yeyote yule hata akiwa mzuri kiaisi gani. Sina hamu naye na wala siwezi kumfanya chochote. Naogopa kusema i hate you women kwani ni kama neno lisilo sahihi.

Nina mke wa muda mrefu sasa na mtoto mmoja, tulioana kwa upendo sana hasa mimi nikiwa na furaha sana kwenye ndoa yangu, lakini cha ajabu mambo yalibadilika sana mara nyingi mke akawa ni wa kulalamika tu, mara nyingi anashinda amenuna, maongezi hakuna kabisa ndani,. Nilijitahidi sana kumuweka chini na kuzungumza naye nikijishusha na wakati mwingine kuomba anisamehe na aniambie makosa yangu yanayomfanya asiwe na furaha.

Mara nyingi nilidhani ni mambo ya "kitandani" labda sifanyi vizuri lakini cha ajabu amekataa sana juu ya hili na kusema anaridhika sana na tena kwa kiwango cha juu na mara nyingi tumekuwa tukifanya hilo tendo hubadilika na kuwa mpole sana na hata kusema ananipenda sana.

Nimemwambia kwa lolote analoona liko tofauti aniambie mara nyingi najishusha sana kwake na nina msikiliza san, lakini nimegundua hana nia ya dhati maana kila kukicha anakuwa vilevile tena wakati mwingine hufanya makusudi kabisa.

Sikutarajia maishani mwangu kuwa na ndoa ya hivi inaniuma sana, nilimuoa kwa taratibu zote za kikanisa na ndoa kubwa na yenye maana, najiuliza kumwacha inakuwa siyo solution maana moyo huwa unaniuma sana kiasi kwamba natoa machozi na kumbembeleza, ninavyoelewa nimefuata moyo wa mama yangu ni mpole saaana tena sana nadhani hata mimi nimerithi huko.

Umefika wakati sasa nimechoka machozi yananitoka kila wakati, ofisini kazi zimenishinda sasa, na siwezi chochote, najihisi sisitahili kuishi duniani lakini natakiwa kuwasaidia wanaonitegemea, nahisi wanawake wote wanaroho mbaya za kinyama kiasi kunitesa hivi, lakini mbona mama yangu ni mtaratibu kiasi hicho? Kuna kitu kimoja kimenijia nimelia sana, nilikuwa namchumba mpole sana ila alinikataa ghafla bila kosa na kwenda masomoni, kumbe hakunikataa ila alifanya hivyo ili tusisumbuane wakati anasoma amemaliza nikiwa nimeoa, aliposikia amelia sana, na mimi nimelia sana. Dunia haijanitendea haki.

Nimetulia chumbani nalia sana saivi sipati solution zaidi moyo wangu unawachukia wanawake zaidi. Wanawake hamna jema kabisa yaani hata mkipendwa na kulelewa kama watoto mnakuwa hivi?



Katiba: Tumeanza Na Mguu Mbaya!

NAUONA mwelekeo mbaya wa upepo wa kisiasa nchini mwetu. Nina shaka kubwa, naamini, tuko wengi wenye shaka na mwelekeo wa nchi yetu tunayoipenda.

Prince Bagenda, Mwakilishi wa CCM kwenye Kongamano la Katiba amekaririwa na gazeti la Mwananchi akitamka; ” Msifikiri kila kitu mnapewa tu, lazima mdai”. (Mwananchi Aprili 3, 2011). Ndio, Prince Bagenda anasema; kuwa hoja ya Katiba haikuwa ya CCM. Kwamba CCM ilikubali kwa kuwa Serikali huongozwa kwa maoni ya wananchi.

Afrika safari ndefu huamuliwa na hatua ya mguu wa kwanza. Ukiianza safari na ’ mguu mbaya’, basi , hiyo haitakuwa safari njema. Ina maana moja kubwa, namna ulivyojipanga na safari yako kuanzia mwanzo. Nilivyofuatilia Kongamano lile la Katiba pale Chuo Kikuu Mlimani, nasikitika kusema, tumeianza safari yetu na mguu mbaya.

Tafsiri yangu juu ya alichokitamka Bagenda ni hii; Katiba ni suala la ’ Sisi na Wao’. Ni mapambano. Hapa kuna tatizo kubwa. Maana, kuna hali ya kutafuta mshindi na mshindwa. Ndio, unatafutwa ushindi na ufahari, le prestige, kama wasemavyo Wafaransa. Ninachokiona, kama tutachagua njia ya kushindana katika kuifanyia marekebisho katiba yetu, basi, hakutakuwa na mshindi. Sote tutashindwa.

Hakika, pale Chuo Kikuu Cha Mlimani ndio tulianza rasmi safari hii ya mchakato wa Katiba kwa wadau kuutolea maoni Muswaada wa Katiba ulio Bungeni sasa. Nionavyo, kama Serikali yetu ni sikivu kweli, na imefuatilia kile kilichoongelewa pale Chuo Kikuu Mlimani, basi, haina kingine, bali kuahirisha safari hii.

Serikali irudi na kutafakari kwa kina. Ndio, safari hii ya kuitafuta Katiba yetu ipangwe upya kwa kuwashirikisha wadau muhimu katika nchi . Na wadau hao tunao. Nayasema haya kama Mtanzania ninayeiangalia na kuitafakari nchi yetu na bendera ya taifa letu . Si chama cha siasa wala bendera yake.

Katika dunia hii, chama na bendera yake huja na kupotea. Nchi na wananchi hubaki pale pale. Si kuna Msajili wa vyama, na anaweza kukifuta chama? Kikapotea chama na wanachama wake. Lakini, duniani hakuna Msajili wa Nchi wala wanachama wake. Ukizaliwa kwenye nchi tayari umeshapata usajili wa kudumu kama mwananchi. Ndio maana, katika nchi za wenzetu, hata raia wao akijiandikisha uraia wa nchi nyingine, bado nchi aliyozaliwa haiwezi kuufuta uraia wa nchi yake aliyozaliwa. Siku yeyote anaweza kurudi nyumbani alikozaliwa na kukaribishwa, awe na hati ya kusafiria ya nchi yake au ameipoteza.

Katika hili la mchakato wa Katiba hii ni rai yangu; ” Tutangulize Maslahi Ya Taifa.” Mifano mingine ni hai na tunaishi nayo. Si tunayaona yanayotokea Ivory Coast? Ni matokeo ya wanasiasa kutotanguliza maslahi ya taifa. Na tumeyaona Misri, Tunisia na kwingineko. Ivory Coast watu wanapoteza uhai kutokana na utata wa matokeo ya Uchaguzi. Chanzo hasa ni mapungufu ya Katiba ya nchi hiyo. Na tuliyaona hayo kwa jirani zetu wa Kenya. Sababu hasa ni wanasiasa wetu kutanguliza maslahi binafsi, ya vyama na makundi yao. Wanasiasa wetu si wepesi wa kujifunza. Ni jukumu letu kuweka shinikizo. Tuweke wazi tunayoyataka kwa nchi yetu. Tusikubali kupitishwa kwenye njia yenye maafa na kubaki kimya. Tuanze kupiga kelele, sasa.

Ni vema na ni busara, kwa kazi ya kuandaa Katiba ya nchi ikaridhiwa na wadau muhimu katika nchi. Inahusu imani. Kukosekana kwa imani kwa maana ya wadau wa Katiba wasipokuwa na imani na dhamira za walioandaa Katiba, basi, hicho huwa ni chanzo cha kinyongo, chuki na machafuko katika nchi.

Haiyumkini mechi ya kandanda ikawa na matokeo ya haki pale timu moja inapojibebesha jukumu la kuamua uwanja, mwamuzi na taratibu za mchezo. Mwamuzi wa kandanda anaweza kuwa chanzo cha wachezaji kupigana uwanjani na hata mashabiki kupigana pia. Mara nyingi chanzo ni upande mmoja kukosa imani na mwamuzi. Kinyume chake, timu zote mbili zikiwa na imani na mwamuzi, basi, mara nyingi mechi humalizika kwa hata aliyeshindwa kutangulia kumpa mkono mshindi na mwamuzi pia. Katiba, mbali ya mambo mengine, iwe pia msingi wa chaguzi za kiungwana ili, kama taifa, tuepukane na yaliyotokea Kenya na yanayotokea Ivory Coast na kwingineko.

Tumedhamiria kuifanyia marekebisho makubwa Katiba yetu. Tufanye hivyo tukiwa na dhamira njema na mapenzi kwa nchi yetu. Nimepata kuandika, kuwa katika hili la Katiba tujiulize; Je, Katiba yetu ya sasa, na kwa wakati uliopo, inakidhi matakwa ya shabaha na malengo yetu kama taifa? Jibu langu ni HAPANA.

Na katika hili hatuna sababu za kugombania fito ilihali nyumba tunayojenga ni moja na ni yetu sote. Ieleweke, kuwa huko nyuma, madai ya Watanzania kupata Katiba mpya yamekuwa ni madai ya haki, muhimu na ya kihistoria. Tumewasikia hata wanaojidanganya, wakiandika, kuwa madai hayo yalitokana na ‘ Njama za Mabeberu!’. Hizi ni propaganda za miaka ya 70, zimepitwa na wakati.

Ni busara kutambua, kuwa wakati umebadilika. Mtanzania wa mwaka 1977 si Mtanzania wa mwaka 2011. Hoja hii ya Katiba si kama nzi anayetua na kuruka. Hoja ya Katiba kwa sasa inaongozwa na kundi kubwa la vijana wanaotaka mabadiliko. Hawa si nzi wanaotua na kuruka, ni siafu wanaokuja kwa kuongezeka idadi yao.

Na harakati za Watanzania kutaka marekebisho ya Katiba zina muda mref. Hizi si harakati mpya. Si harakati za chama au kikundi kidogo cha ’wapinzani’ wasioitakia mema nchi hii. Siku zote, yamekuwa ni madai ya msingi ya Watanzania, bila kujali tofauti zao za kiitikadi, kidini, rangi na makabila.

Kama ni shauri mahakamani, basi, lilishafunguliwa zamani. Kinachofanyika sasa ni mwendelezo wa shauri. Si wengi, miongoni mwa vijana wa sasa, wenye kumbukumbu ya ukweli huu. Kuwa tayari mwaka 1991 vuguvugu la kudai vyama vingi na Katiba mpya lilishaanza. Wakati huo madai makubwa yalikuwa mawili; vyama vingi na Marekebisho ya Katiba. Kuna mnaokumbuka ’ KAMAKA’- Kamati ya Marekebisho ya Katiba iliyoundwa na wanaharakati. Ikumbukwe, kuwa hayo yalikuwa ni madai ya Watanzania ndani ya mfumo wa chama kimoja.

Marehemu Chifu Abdalah Fundikira aliongoza Kamati iliyoundwa, si na Serikali, bali wanaharakati, kuratibu mchakato wa kudai vyama vingi na Katiba mpya.

Hata wakati huo, Mzee Mwinyi, kama Rais, aliweka ‘ mkwara’, kuwa madai hayo yasiendeshwe na watu au makundi ya watu bila kibali cha Serikali. Presha ya madai ilipoongezeka, tunakumbuka, kuwa Mzee Mwinyi aliweza kusoma alama za nyakati. Aliongea pale Chuo Kikuu Mlimani na kuweka bayana dhamira ya Serikali ya kuunda ‘ Tume ya Nyalali’ . Tume hiyo ilizunguka nchi nzima kuwauliza Watanzania kama wanataka kuendelea na Chama kimoja au Vyama vingi.

Itakumbukwa, Chifu Fundikira alipata kutamka; kuwa huko ni kupoteza muda na fedha za wananchi. Itakumbukwa pia, Mabere Marando alikuwa Katibu wa Kamati ile ya wanaharakati ya kuratibu mchakato wa madai ya kuwepo na vyama vingi na marekebisho ya Katiba. Marando alipata kutamka na kunukuliwa na Daily News, April, 12, 1991; “ We have a bad political system because our Constitution embraces political discrimination. What we want is that all of us should shout out that our Constitution is bad.” ( Mabere Marando, Daily News, April 12, 1991)

Tafsiri; “ Tuna mfumo mbaya wa kisiasa kwa sababu Katiba yetu ina ubaguzi wa kisiasa. Tunachotaka, ni sote, tupige kelele, kwamba katiba yetu ni mbaya.”)

Marando aliyasema hayo katika Semina ya kwanza ya Kamati ya kuratibu mchakato wa madai ya vyama vingi na Katiba mpya iliyoongozwa na Chifu Fundikira. Semina hiyo iliudhuriwa na watu wapatao 800 kwa mujibu wa taarifa ya Daily News la April 12, 1991.

Na akina Chifu Fundikira waliandamwa sana na Serikali na Chama Tawala. Kwa mujibu wa Daily News la April 26, 1991, Mbunge wa Shinyanga, Ndugu Paulo Makolo alimshambulia Fundikira kwa kusema kuwa , katika hilo la kuwa na vyama vingi na katiba mpya , Chifu Fundikira hakuwakilisha mawazo ya Wasukuma na Wanyamwezi wenzake; “ This is not a Wanyamwezi and Wasukuma movement. It is the selfish interests of Fundikira and his ten colleagues. Our people are not after parties. They want food, water, education and health care.” ( Paulo Makolo, MP, Shinyanga, Daily News, April 26, 1991).

Mwenyezi Mungu umrehemu Chifu Abdalah Fundikira. Nahitimisha.

 

 

ACHA KUSUBIRI MWANAUME AKWAMBIE ANAKUPENDA,KAMA UNAMPENDA MWAMBIE.....

Hili mnalizungumziaje wadau?
Mwanaume...mwanamke akikufata kukwambia anakupenda utaichukuliaje?
Mwanamke...kama kuna mwanaume unampenda utamfata kumwambia?utasubiri yeye akufate?na kama hajui kama una hisia juu yake utafanya nini ajue hilo?

NI KWELI MVUA INALETA HAMASA YA NGONO??

Kwa sasa mvua ina nyesha...kuna mtu kanifata ananiambia mpenzi wake ana mwambia awahi kutoka ofisini leo kwani ana hamu nae na hiki kimvua ndo usipime.Akaniuliza hivi mvua huwa inaleta hamu ya kufanya ngono?mie sikuwa najibu kwa sababu mie binafsi huwa napenda kulala wakati mvua inanyesha nje.Nikasema nikuulize mdau ni kweli haya mambo mvua huleta hamu na kama ni kweli kwa nini??

KUMPOTEZA MTU ULIE MPENDA SANA KUNAWEZA KUBADILI KABISA MAISHA YAKO!


MIMI NI KIJANA UMRI WANGU NI MIAKA 25 NINA TATIZO AMBALO LINANITESA SANA.

BAAADA YA KIPENZI CHA ROHO YANGU KUFA GHAFLA NIKAANZA KUWA KAMA ABNORMAL YAANI NIKAANZA KUOGOPA SAANA NAKUWAZA VITU AMBAVYO LABDA NAHISI NAUMWA NIKAANZA KUHISI KWAMBA NA MIMI NAUMWA UGONJWA ULEULE WA MAREHEMU NAANZA KUTEMBEA NA MTU NAONA KAMA SAA YOYOTE NTAKUFA NAPENDA KUWA KARIBU NA HOSPITAL NA NINAAMINI KTK MADAKTARI PIA.


NIKASHINDWA KWENDA KAZINI NAOGOPA KUPANDA MABASI NAOGOPA KILA KITU NAONA KAMA NAKUA KICHAA NASKIA KAMA MOYO UNAENDA MBIO, NASKIA KAMA PIN ZINANICHOMA KICHWANI NA MIGUUNI NASKIA KAMA HATA FUTURE HAIPO KUNASAAA NAKUA DUUUM YANI KAMA NAWAZAAA LAKINI SIJUI NACHOKIWAZA NATOA JASHOO MNOO LAKINI UKIPIMA KILA KITU NIPO SAWA KABISA NILIKUA OVER FEAR OF EVERY THINGS.

NAOMBA MLIZUNGUMZE HILI KWENYE KIPINDI CHENU CHA (LEO TENA) PLS NAOMBA NIJUE NITASAIDIWAJE. SWALI HALI HII ITAISHAA? NA NINAWEZA KUIMALIZAJEE? NA JEE NTAKUFAAA?

BARANI AFRIKA:- UTAMADUNI WA KUSIMULIA HADITHI BADO NI MUHIMU!!!

Hadithi kama tujuavyo ni njia ya maridhiano isiyo na gharama na ya kudumisha utamaduni.

Wengi wetu tunakumbuka nyakati ambazo wazazi au mababu na mabibi zetu walipokuwa wakitusimulia hadithi za kufurahisha zilizotokea zamani. Nilipoiona picha hii nimekumbumbuka sana zamani nilipokuwa mdogo wakati wa jioni wote mnakusanyika na kusikiliza hadithi na hapo hapo mnamenya karanga au kupukuchua mahindi na hapohapo mnaota moto....

 MDALASINI, TANGO NA ASALI....





jamani wenzangu nina jambo mlikuwa mnajua kama mdalasini, asali na tango ni dawa ya kumpa mtu nguvu kwenye mechi? kama ulikuwa hujui ndio ufahamu eti..


kuna dada mmoja alikuwa analalamika mpenzi wake nguvu kitandani hana, anasema jamaa akishatoa moja tu basi nguvu zote zinaisha jamaa hawezi hata kurudia ya pili, na hapo mwanamke wake huyo anakuwa hajatosheka lakini jamaa hajiwezi kabisa..


sasa huyu dada akawa anaomba ushauri kwa watu wazima akiwaeleza swala lake na mumewe watu wengi wakawa wanamshauri mengi tu pamoja na ya kwamba mumewe anywe maji ya mchele yale ya kwanza, sijui mwengine akamwambia anywe maji ya madafu kwa wingi na wengine wakimwambia aende kutafuta dawa za miti shamba...

akafika kwa bibi mmoja wa zamani (umri umeenda) yule bibi akamwambia yule dada ampe mumewe mdalasini pamoja na asali achanganye kwa pamoja atie na maji ama aiweke kwenye chai, halafu kila chakula cha yule baba kisikose kipande cha tango..
yule dada akafanya kama alivyoambiwa na yule bibi, sasa hivi dada anafuraha mambo si shwari, kwahiyo huu ni ushauri tu ya kwamba ukiona mwezio nguvu hana akienda moja anahema kama kasukuma trekta, mwanaume anahema kama presha imeshuka (hehehe) basi sio vibaya ukijaribu hayo..
lakini naomba niseme sio tu kwasababu huyu dada yeye mpenzi wake alipata nafuu ndio kila mtu itakuwa hivyo wengine vyao vya kurithi utalisha hivyo vitu milele jamaa hata kubadilika asibadilike...

 Ninasoma "Siku ya Watenzi Wote"

Kwa siku kadhaa sasa nimekuwa nikisomaa Siku ya Watenzi Wote, kitabu cha Shaaban Robert, ambacho nilikinunua tarehe 8 Julai pale Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili, Chuo Kikuu Dar es Salaam, kwa bei ya shilingi 5,000 tu.

Ninapenda kusoma vitabu muhimu kama hivi vya Shaaban Robert, kama nilivyoandika katika blogu hii na katika kitabu cha CHANGAMOTO. Nimeamua kujieliDisha ili niweze kuandika kwa ki-Swahili vizuri iwezekanavyo. Ni jitihada binafsi ya kujikomboa kutokana na kasumba na fikra potofu tulizo nazo wengi, hasa wasomi, kuhusu lugha ya ki-Swahili. Ninataka kuonyesha heshima kwa lugha hii kwa kuiandika kwa usahihi.

Mambo mengi yaliyomo katika Siku ya Watenzi Wote yanatokea Dar es Salaam. Tunawaona wahusika wakiwa katika mitaa kama Kichwele, Ilala, Mnazi Moja, Kariakoo, na Msasani. Hii inafurahisha, kwani mwandishi anauenzi mji huu kwa kuuweka kitabuni namna hii. Inanikumbusha hadithi za mwandishi Moyez Vassanji, kama vile Uhuru Street, ambaye naye aliandika sana kuhusu Dar es Salaam.

Katika Siku ya Watenzi Wote, ambacho kinasemekana kuwa ni kitabu chake cha mwisho, Shaaban Robert anarejea katika masuala ambayo alikuwa ameyashughulikia katika maandishi yake yaliyotangulia, kwa miaka mingi. Shaaban Robert anaongelea na kutafakari masuala muhimu ya jamii, kama vile tofauti za matabaka, tabaka la maskini na tajiri, hali ya wanawake. Tunamsikia Shaaban Robert mwanafalsafa, mchambuzi wa masuala ya jamii, mwenye hisia nzito kuhusu maana ya maisha, mahusiano baina ya wanadamu, haki, na utu. Shaaban Robert anawakosoa walimwengu kwa ufinyu wa mawazo ambao tunauendekeza kwa kisingizio cha dini.

Kitabu kama Siku ya Watenzi Wote ni hazina kubwa. Kila ukurasa una mambo ya kugusa akili na hisia, kupanua mawazo na ufahamu wa lugha. Thamani ya kitabu kama hiki ni kubwa mno, wala haipimiki kwa fedha, hata kama kingeuzwa kwa shilingi 50,000

 Barua za Shaaban Robert

Kitabu cha Barua za Shaaban Robert ni mkusanyiko wa barua alizoandika Shaaban Robert kwa mdogo wake Yusuf Ulenge baina ya mwaka 1931 na 1958. Yusuf Ulenge alifanya busara ya kuzihifadhi na sasa zimechapishwa kama kitabu, na Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Mhariri Profesa Mugyabuso Mulokozi amefanya kazi kubwa na watafiti wenzake katika kuzichapisha na kuziwekea maelezo.

Nilikinunua kitabu cha Barua za Shaaban Robert mwaka 2008 katika duka la Taasisi. Nilifurahi na pia kushtuka kugundua kuwa Yusuf Ulenge alikuwa mdogo wa Shaaban Robert. Jina la Yusuf Ulenge nililifahamu tangu kwenye mwaka 1964, nilipokuwa darasa la sita. Nilinunua kitabu kiitwacho Nguzo ya Maji na Hadithi Nyingine, kilichotungwa na Yusuf Ulenge. Miaka yote sikuwa na wazo hata kidogo kuwa huyu alikuwa mdogo wa Shaaban Robert.

Sasa, hizi barua zimenifungua macho kabisa, kwani nimejionea jinsi uhusiano wa hao ndugu wawili ulivyokuwa mkubwa na jinsi Yusuf Ulenge naye alivyokuwa mwandishi mahiri. Katika kitabu hiki kuna taarifa za maandishi mengi ya Yusuf Ulenge, vikiwemo vitabu alivyochapisha na vingine alivyopangia kuchapisha. Mzee Yusuf Ulenge alifariki tarehe 16 Desemba, 2002.

Shaaban Robert ni mfano wa mlezi bora, kwa jinsi alivyokuwa anamshauri na kumwongoza mdogo wake Yusuf katika masuala mbali mbali ya maisha, kama vile elimu. Siwezi kuelezea kwa ufasaha jinsi Shaaban Robert alivyothamini elimu na maadili mema, akawa anamwongoza Yusuf katika njia hiyo. Shaaban Robert alikuwa tayari kutoa gharama zozote zilizohitajika kumlipia Yusuf katika masomo yake, kuanzia daftari hadi usafiri. Ni mfano mzuri sana kwetu wazazi na walezi wa watoto.

Kitabu hiki kinaelimisha sana. Kinautikisa kabisa moyo wangu kwa undani na uzito wa maudhui yake. Kitabu hiki kinafaa kuwemo katika kila nyumba ya wa-Tanzania, ili kisomwe na wazazi na watoto. Hakuna kisingizio cha kutokuwa na kitabu kama hiki, na vitabu vingine vya Shaaban Robert, ambaye ndiye gwiji wa uandishi wa ki-Swahili, mwanafalsafa na mwalimu wa jamii. Hayo nimeyaelezea katika kitabu cha CHANGAMOTO: Insha za Jamii, uk. 30-41

Ingekuwa ni hapa Marekani, tukio la kuchapishwa kitabu kama hiki lingekuwa na kishindo, na watu wangepanga foleni kwenye maduka ya vitabu kukinunua. Kingezungumziwa magazetini na vyombo vingine vya habari. Wa-Tanzania tunapaswa kujiuliza iweje hatuna utamaduni wa aina hiyo. Iweje hatuna hata habari wala hamu ya kujua mwandishi kama Shaaban Robert alizaliwa wapi na aliishi wapi na mchango wake katika jamii na ulimwengu ni upi. Tuko wa-Tanzania yapata milioni arobaini. Ni nyumba ipi katika Tanzania, kuanzia nyumba za walalahoi hadi za hao tunaowaita viongozi, yenye vitabu vya mwandishi muhimu kama huyu?

Kwenye mtandao wa Facebook kuna ukumbi wa wadau na wapenzi wa Shaaban Robert, uitwao Ukumbusho wa Shaaban Robert. Walioanzisha ukumbi huu si wa-Tanzania, bali wa-Kenya. Hii ndio hali halisi, kwamba nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake. Kuthibitisha zaidi jambo hili, jionee jinsi mwanafunzi m-Marekani alivyokichangamkia kitabu hiki cha Barua za Shaaban Robert, akakiandikia uchambuzi huu hapa.

 JINSI YA KUPUNGUZA MAJI MAJI KATIKA VIUNGO VYA UZAZI WA MWANAMKE

 


 Nina umri wa miaka 28 na nina watoto 2. Tatizo nililonalo sasa ni uke kuwa na majimaji yaani sio mkavu, japo haukuwa mkavu sana hapo awali nilikuwa wa kawaida.
Tatizo lilianza mwaka jana baada ya kujifungua mtoto wa pili uke umekuwa na majimaji hata kunifanya nisifurahie tena tendo la ndoa japo mume wangu hajawahi kuongelea jambo hili ila nahisi hata yeye hafurahii kama hapo awali.

Naombeni msaada kwa yeyote mwenye kujua dawa ama nini cha kufanya ili uke uwe mkavu ili ninusuru ndoa yangu jamani.

USHAURI

Umesema uke wako una majimaji na hivyo haufurahii tendo la ndoa, unahisi pia mume wako hafurahii, na hivyo unaomba dawa ili kuinusuru ndoa yako.
Kwa kawaida kwa wanawake ambao wameshavunja ungo na bado hawajaingia uzeeni (menopause) ukeni mwao huwa si kukavu,(na kama wakipatwa na ukavu ukeni basi wanahitaji tiba) na umajimaji au unyevunyevu huo ni muhimu sana na unakazi yake maalum, na huzidi vipindi fulani Fulani - nitaeleza.

Hata hivyo kwa kuwa wanawake wanatofautiana ni vigumu kusema ni kiasi gani cha umajimaji huo ni wa kawaida na upi umezidi. Hata hivyo namiini mwanamke ambae anahitaji kuvaa pad wakati hayuko kwenye menses hali hiyo inahitaji kuchunguzwa. (Wewe hukusema ni kiasi gani)


Kiutalaamu zipo sababu nyingi zinazofanya uke uwe na unyevunyevu, sababu zingine ni za kibaologia (za kimaumbile) na hivyo hazihitaji tiba, zingine zinaletwa na maradhi, na sababu nyinginezo.

• kibiologia, hutokea mara baada ya kuvunja ungo, unyevunyevu wake huwa haunuki, hauwashi, haunguuzi na haufanani kabisa na usaha. Unyevunyevu huo huzidi wakati wa msisimko wa ngono, na au wiki ya pili au ya tatu baada ya siku zako, na au kama unatumia baadhi ya dawa za majira nk.

• Maradhi: majimaji yake huwa yanaharufu, kama usaha,au ya kijani au kama maziwa yaloganda au kama povupovu.  

Husababishwa na uambukizo wa trichomonas, fungus, kisonono nk , pia maradhi kama fistula (nasuri), au polyps yaweza sababisha hali hiyo. Pia maradhi kama kisukari yaweza leta hali hiyo.

• Sababu nyingine, Douches (kujipiga bomba ukeni), kusafisha uke kwa sabuni au kemikali nyingine, kuingiza manukato ukeni, kutumia condom (baadhi ya wanawake),kuvaa nguo zinazobana sana na hivyo maeneo hayo kukosa hewa nk.

Kwa kuwa sababu ni nyingi nakushauri nenda hospitalini ukachunguzwe kabla hujatumia dawa yoyote kwa sababu huenda ni kawaida au huenda ni maradhi. Na kama ni ugonjwa kila ugonjwa una tiba yake.

Na wakati unajiandaa kwenda hospitali nakushauri usifanye douches, usijisafishe ukeni na sabuni au kemikali yoyote, vaa nguo za pamba ambazo hazikubani.

 

JINSI YA KUAMUA KUZAA MTOTO WA KIKE AU WA KIUME.... SOMO HILI LITASAIDIA KUPUNGUZA UGOMVI


USHAURI JINSI YA KUPATA MTOTO WA KIUME AU WA KIKE:
Naomba ushauri wa kujua jinsi ya kuamua kupata mtoto wa kiume au wa kike. Cha muhimu ni kujua wakati gani nikikutana na mke wangu atakuwa na mimba ya mtoto wa kiume au wa kike?

 Mimba inaingia siku ya 12 hadi 15 toka siku ya kwanza ya hedhi.

Mfano mwanamke anaingia kwenye hedhi tarehe 3 may basi huyu atashika mimba tarehe 15may hadi tarehe 18may maana tarehe 15may ni siku yake ya 12. 

Sasa basi ukitaka mtoto wa kike basi tembea na mkeo tarehe 14may siku ya 11 ambayo kwa kawaida sio siku ya mzunguko ya kupata mimba. 
Mbegu za watoto wa kike zinachelewa kufa ndani ya uke.

Mbegu zinazoleta mtoto wa kike hufa ndani ya uke baada ya masaa 24 lakini mbegu zinazoleta mtoto wa kiume hufa baada ya masaa 4 na zina nguvu kwelikweli maana ukipiga bao moja linatosha kuzalisha .baada ya  muda huo bao hilo  halizalishi maana nguvu yake inakuwa imeisha. 

Kwa kifupi kuna vitu vingi vinavyoungana kwa pamoja .Kuna kunawa baada ya tendo.

Mwanamke asinawe kabisa maji ya baridi maana ataathiri mwendo wa mbegu hizo. 

Akilazimika kunawa basi yawe maji ya moto. Jaribu njia hii utafanikiwa kumpata mtoto unaemtaka..

Facebook Au Fitnabook

Kwanza kabisa, ijulikane wazi kwamba kusudio la makala hii si kutoa fatwa wala hukumu. Lengo ni kuweka wazi manufaa na madhara ya Facebook ili mtu binafsi atoe hukumu yake mwenyewe.
Je, ni Facebook au Fitnabook? Hili ni suali ambalo watu wengi wameanza kujiuliza baada ya kujionea  vitimbi na kashfa kadhaa katika huu mtandao ambao unazidi kujipatia umaarufu kila pembe ya dunia. Naam, kuna vitimbi kadhaa vinafanyika kwa jina la Facebook. Na ndio kuna vijana wengi ambao wametumbikia katika janga la fitna katika Facebook lakini nini suluhisho la hili?Kabla hatujatazama hebu kwanza tuangalie manufaa na madhara ya Facebook.
Manufaa
Kama ilivyo kawaida ya vitu vingi, Facebook ina faida yake. Lakini je, hizo faida ni nyingi kuliko madhara? Katika sehemu hii tutaja manufaa ambayo yako wazi kutokana na utumiaji wa Facebook. Manufaa hayo ni kama yafuatayo:
1.     Kufanya da’wah ( kuwalingania watu kwenye Uislam)
Madaa’iyah kadhaa pamoja na baadhi ya Mashaykh hutumia Facebook kwa kazi za da’wah. Huwekwa na kutumwa vitu mbalimbali vya kufikisha mafunzo mbalimbali ya Dini kama: video za mawaidha, makala za Kislamu na njia mbalimbali za kunufaisha wasomaji.
 2.     Kuwasiliana na jamaa na marafiki wa mbali
Mara nyingi watu hutumia Facebook kwa kuwasiliana na jamaa zao ambao wanaishi nje ya nchi kwa hoja ya kwamba ni njia rahisi na ya nyepesi ukilinganisha na njia nyinginezo. 

3.     Kutangaza shughuli na harakati za Kiislam

Ijtimai na mikusanyiko mingi ya Kiislamu na mambo yanayowahusu Waislamu mara nyingi huwa yanatangaziwa kwa kutumia Facebook. Njia hii pia inaruhusu waandaaji kujua watu wangapi watahudhuria au kupatikana katika shughuli au harakati zao.
 Madhara 
Ijapokuwa kuna manufaa kadhaa juu ya utumiaji wa Facebook, kuna balaa na fitnah nyingi hupatikana humo, kadhalika watu wengi wanaitumia kwa njia mbaya. Katika madhara ya Facebook ni haya:
 1.     Kupoteza muda kwa mambo ya upuuzi
Watu wengi hasa vijana hupoteza masaa juu ya Facebook wakati wangeliutumia muda ule kwa kufanya kitu cha muhimu.

2.     Mchanganyiko wa wanaume na wanawake
Ada kuu iliyoshamiri na kuenea kati ya watumiaji ya Facebook ni kutazama na kuongea na watu wasio Mahram zao.

3.     Kutokewepo kwa hayaa na heshima
Uislamu umekuja kulinda heshima ya binaadam lakini cha ajabu vijana wengi wa Kiislamu hutokwa na hayaa na huvuruga heshima zao kupitia Facebook. Wasichana wangapi wameweka picha zao bila ya hijaab kwenye Facebook kwa kutaka kujionyesha? Wanawake wangapi wameharibu heshima zao na za familia zao kwa kutuma maasi yao kwenye Facebook?
 4.     Kukashifiwa Mtume na Uislam 
Kubwa zaidi na baya zaidi na la hatari zaidi, ni hili lililotokea majuzi la kukashiwa kwa Mtume kwenye Facebook, jambo ambalo limewasikitisha wengi wetu na tuna kila haki ya kuhuzunika juu ya hilo. Picha mbalimbali za kashfa na za kumlinganisha Mtume wetu mtukufu Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na mambo maovu na machafu, zimewekwa huko kwa kuchorwa vikatuni vinavyodaiwa kuwa ni yeye. Na yamejitokeza makundi tofauti yaliyoungana huko kwenye Facebook ili kuukashifu Uislamu na Waislamu na kumdhalilisha Mtume wetu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Haya yote ni matunda ya hiyo Facebook.

 Suluhisho 
Baada ya kujionea na kutafakari juu ya madhara na manufaa yaliyomo kwenye Facebook, lilobakia ni kujiamulia mwenyewe. Ikiwa utaona kwamba Facebook madhara yake ni makubwa kuliko faida, basi ni juu yako kujihadhari juu ya kuitumia na bora zaidi kujiepusha nayo. Ikiwa utaona kwamba manufaa yamezidi basi ni pia juu yako kujichunga na madhara yaliyomo huko. Inawezekana kitu ukakiona kina manufaa kadhaa lakini madhara yake ni mengi zaidi. Allaah Anasema kuhusu ulevi na kamari
 Udini na ukabila ni ufa mkubwa unaobomoa utaifa Tanzania

MOJA ya hotuba za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere zisizochujuka ni ile aliyoitoa hoteli ya Kilimanjaro mbele ya Klabu ya Waandishi wa Habari Tanzania Machi 13 Machi 1995.
Katika mazungumzo yake , Mwalimu alitaja nyufa tano  zinazolitikisa taifa letu kuanzia kwenye paa, katika dari, kwenye kuta hadi kufikia katika msingi ule imara wa taifa uliojengwa kwa muda mrefu.
Alizitaja nyufa hizo kuwa:- muungano, kupuuza na kutojali, kuendesha mambo bila kujali sheria, rushwa  na udini na ukabila.
Katika makala  hii nitajikita zaidi katika huo ufa namba tano, ambao ni udini na ukabilaTanzania. Nimechangamshwa na mawazo endelevu ya ile makala ya  Elias Msuya katika gazeti  hili, toleo la  Jumapili, Juni  24, 2012 ukurasa wa 11.
Msuya alikuwa anajibu tuhuma zilizotolewa na Thuway Owaray kupitia Mwananchi la Juni 17, 2012.
Katika makala yake, Msuya amezungumzia kuhusu Sensa na Mahakama ya Kadhi, kadri yanavyochukuliwa na waumini wa Kiislamu.
Kwa muda mrefu sasa, tuseme miaka nenda miaka rudi  nchini mwetu kumesikika malalamiko au manung’uniko ya wafuasi wa dini moja kudai kukandamizwa au kunyimwa fursa sawa za elimu katika nchi yetu.
Mfumo wa elimu umeonekana kuwakandamizi na Serikali iliyoko madarakani haifanyi lolote kuondoa uonevu wa namna hiyo.
Mfano ni ile makala ya Abufirdaus aliyetoa malalamiko katika gazeti moja la kila wiki Rai , Aprili 22 – 28, 2004 iliyokuwa na kichwa cha habari, 'Kweli udini Tanzania upo,tujirekebishe'.
Aidha, yalitolewa  madai  ya haki za Waislamu kama yalivyotolewa na kauli ya Baraza Kuu la Jumuia  na Taasisi za Kiislamu Tanzania mwaka 1993. Mwaka 1998 kulitolewa 'wasilisho' kwa Serikali kulaumu Kanisa Katoliki na Serikali ya CCM katika hili. Kuna malalamiko yanayojirudia rudia licha ya kutolewa majibu na mamlaka husika. Ndipo ninajiuliza kwani kulikoni?
Daima yanazuka malalamiko ya namna ile ile na hawa ndugu zangu, rafiki zangu, Watanzania wenzangu wanazuoni wazuri tu kwa nini hawaridhiki? Huenda kuna jambo linatafutwa.
Nikasema hebu nijaribu kuelezea kihistoria na kimila na utamaduni wa Kibantu, labda itasaidia kuona kiini cha yote haya ni nini?
Kwanza, niwarudishe nyuma wasomaji wangu hasa vijana mwaka 1962 baada ya Mwalimu Nyerere kula kiapo cha urais wa Jamhuri ya Tanganyika. Mwalimu Nyerere alipokuwa analihutubia Bunge ukumbi wa Karimjee,Desemba 10, 1962 alikuwa na maneno haya kwa wananchi wote.
“…kwa mfano, uhasama baina ya waumini wa Kiislamu na Kikristo ambao unaweza kuenezwa na fikra potofu ; kama tunavyojua, ni matokeo ya serikali ya kikoloni kutojihusha hata kidogo na elimu kwa Waafrika na kwa maana hiyo wengi wa wale walioipata kwa kiwango chochote, walifanya hivo kupitia shule za misheni na kwa hiyo ni Wakristo, hivyo wengi wao ni Wahaya, Wanyakyusa  na Wachagga.
(Hotuba ya Nyerere: akilihutubia Bunge la kwanza la Jamhuri ya Tanganyika ,Desemba 10 1962; tazama- Uhuru na Umoja uk. 179).

Maneno haya yanaonyesha kuwepo kwa tatizo la kielimu baina ya Wakristo na Waislamu na pia kuwa yapo makabila yaliyonufaika zaidi kielimu kuliko mengine katika nchi yetu.
Aidha, lipo onyo la msingi kuwa, watakuwepo wakorofi na wasiokuwa na nia njema kwa uhuru wetu watakaotumia hali hiyo kuchochea manung’uniko na kuleta mtafaruku miongoni mwa wananchi huru.
Na ndivyo inavyotokea sasa watu namna hiyo wanalalamika udini na dhuluma katika kupewa elimu hapa kwetu. Baba wa Taifa kwa kuona mbali juu ya suala hilo alilipa dawa pale aliposema, “hakuna njia rahisi ya kuondoa upungufu huu katika elimu kati ya Wakristo na Waislamu…”
Katika hotuba yake ile ile ya Desemba 10 , 1962 (taz. Uhuru na Umoja uk. 181). Mwalimu hakukomea kusema hayo tu bali kama sote tunavyojua, mwaka 1970 Serikali ilitaifisha shule zote za misheni na za binafsi katika nchi yetu kama hatua muhimu ya kupunguza tofauti katika elimu kwa Waislamu na Wakristo maana kuanzia hapo hapakuwepo tena shule za misheni. Matokeo ya utaifishwaji ule, yameharakisha sana upatikanaji wa elimu dunia kwa Waislamu wengi hapa nchini.
Hii ilikuwa njia ya kusawazisha upatikanaji wa elimu kwa watoto wote wa Tanzania kwa kuwalea pamoja ili wajitambue ni watoto wa taifa moja.
Kwa upande wa Tanzania visiwani , shule zote wanafunzi wake  wengi niWaislamu na kila msichana anavaa hijaabu kama sare, hakujasikika Wakristo wakisema kuna udini, na wanabaguliwa kwa misingi ya dini. Elimu dunia haina dini. Ni utamaduni uliozoeleka kule visiwani tangu enzi za Sultani.
Pia, ni vema tukakumbuka maneno ya Alhaji Ally Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili aliyoyatoa siku akifungua ofisi za Shirika la World Muslim League mwaka 1998 hapa Dar es Salaam, alitamka hivi “… Ndugu Waislamu, punguzeni malalamiko dhidi ya Serikali na muanze kufanya kazi… tujenge vyuo vya elimu ya kizungu ili tuwaandae watoto wetu kushika nafasi za uongozi…”
Je, kuna mwongozo bora na safi kuliko huo? Mbona Zanzibar kunajengwa vyuo kadhaa vya waislamu? Kwanini hapa Tanzania Bara tunarudia rudia lalamiko lile lile la kubaguliwa kwa misingi ya dini wakati Serikali ilikwisha futa shule za dini?
Kwa nini zisitolewe takwimu za vyuo na shule ngapi wakereketwa na wanaharakati Waislamu wamejenga kuandaa watoto wao kwa kushika uongozi?
Mwaka huu, 2012  limeibuka lalamiko la matokeo ya mtihani wa Kidato cha Sita kwa shule za Waislamu hata kuwafanya wengine wasiwe na imani na uongozi wa Baraza la Mitihani (NECTA).
Naona maelezo yaliyotolewa na Sadiki Godigodi yanatosheleza. Huyu ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Islamic Peace Foundation ametoa maelezo ya kueleweka sana katika gazeti la kila siku Majira la Jumatatu, Juni 25 , ukurasa wa 3. Ameeleza wasahihishaji wanaona namba za watahiniwa wala siyo majina yao, hivyo wasahihishaji hawajui karatasi hii ya Mwislamu au ya Mkristo! Aidha, amekazia kuwa kamati mliyoiamini imefanya kazi kubwa na nzuri na uchunguzi wao umeonesha wazi kuwa hawakulenga kuwafelisha wanafunzi waislamu. Somo walilofeli zaidi ni Islamic Knowledge.
Sadiki akaonya kuwa wote wanaonufaika na mgogoro huo waache fitina na kueneza chuki ambazo hazina misingi.
Siku za nyuma malalamiko ya mitihani yaliwahi kutokea 1988 – 1990 na lilivuja dokezo la Wizara ya Elimu kwa Rais Mwinyi la Oktoba ,10,1988 lenye kuonyesha takwimu za watoto waislamu waliochaguliwa/walioteuliwa kuingia kidato cha  kwanza na wale waliochaguliwa kuingia chuo kikuu, kuthibitisha wanavyokandamizwa kwa mfumo wa elimu uliopo.

   WAZAZI HUCHANGIA WATOTO KUKOSA AKILI DARASANI

Uchunguzi wa kitaalamu uliofanywa na baadhi ya mashirika yanayojihusisha na malezi ya watoto ulimwenguni akiwemo Daktari Janet Gonzalez Mena wa Marekani, umebaini kuwa wazazi ndiyo mwanzo hasa wa mafanikio ya watoto wao na kwamba wengi kati ya vijana wanaoshindwa katika maisha kushindwa kwao kunaanzia ndani ya familia zao.
Malezi ya wazazi kwa tafsiri sahihi ndiyo yanayomkuza mtoto na kumtambulisha katika jamii kwamba yeye ni nani? Tunawapata watu wa kabila la Wanyamwezi, Wayao, Wamakua, Wamakonde kwa sababu wamezaliwa na kulelewa na wazazi wa makabila hayo.

Pamoja na yote, kuzaa peke yake bila ya kusimamia tabia ya mtoto huwa ni kazi bure. Waswahili husema: “Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.” Kwa bahati mbaya wazazi wengi wamekuwa hawaelewi kuwa wao ndiyo wenye jukumu la kumtayarisha mtoto awe mwema na mwenye uwezo wa kufikiri.
Hali hii inatokana na kutokuwepo kwa elimu inayotoa somo la jinsi ya kuwalea watoto bila kuwaharibia ufahamu na kuwadumaza katika uelewa wa mambo.

Jambo la kusikitisha ni kwamba, wazazi ambao ndiyo wenye uchungu na watoto wametajwa kuwa chanzo cha watoto kushindwa kukabiliana na changamoto za kimaisha pamoja na masomo.
Ukichunguza kwa makini watoto wengi wanaokuwa mbumbumbu darasani (nazungumzia wale wasiokuwa na kasoro za kibaiolojia) ni wale ambao wazazi wao hawakuzingatia mambo yafuatayo katika kuwalea tangu walipokuwa wadogo hadi kukua kwao.

 HUDUMA BORA
Wazazi wengi hasa wa dunia ya tatu wanakabiliwa na tatizo la uzazi holela, usiozingatia uwezo wa kulea na kuwapa huduma muhimu watoto wao. Mfano lishe bora, mavazi na malazi. Wanasayansi wanasema chakula bora ndicho kinachoweza kuimarisha ukuaji wa viungo vya mtoto na kuufanya ubongo uwe katika hali nzuri ya kumudu kutafsiri mambo.
Hivyo ni jukumu la mzazi anayetaka mtoto wake awe na uelewa mzuri darasani ahakikishe kuwa anampatia mwanae chakula bora kitakachomjenga afya na kumuwezesha kuwa na mwili wenye nguvu ya kukabili magonjwa ya kitoto. Lakini sambamba na hilo mzazi anatakiwa kusimamia afya ya mwanae kwa kumpeleka hospitalini mara kwa mara kutibiwa na kushauriwa.

UTAMBUZI WA KIPAJI
Jambo la pili ambalo ni muhimu kwa mzazi ni kutambua mapema kipaji cha mtoto na kumuongoza sawa na kipaji chake. Ingawa shule nyingi nchini (Tanzania) hazitoi elimu ya ngazi ya chini lakini baba na mama bado wanawajibika kujua ni elimu ya kiwango gani kutoka shule gani itamfaa mtoto wao.
Inashauriwa kwa mzazi kumtambua mwanae ana uelewa gani, ili ajue namna ya kumsaidia ili afikie kiwango bora cha uelewa.
Kwa mfano, mtoto akiwa na uelewa wa chini anatakiwa kupelekwa kwa waalimu wazuri wenye uwezo wa kumsaidia anaposhindwa, haifai mtoto wa aina hii kupelekwa shule za ilimradi na kudhani huko atasoma na kuelewa.
Itaendelea wiki ijayo.
Masomo haya ya jinsi ya kumsaidia mwanafunzi wa ngazi yoyote kuwa wa kwanza darasani yanapatikana pia kwenye kitabu changu cha saikolojia, mbinu za kusoma na kufaulu mitihani kinachopatika Dar es Salaam pekee kwa wauza magazeti.

 Hongera Basata kwa mikakati hii

BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) na asasi ya Gaba Arts, mapema wiki hii waliendesha semina fupi kwa wasanii wa filamu iliyohusu kuwajengea weledi katika eneo la uandishi bora wa miswada ya sinema (script writing).
Semina hiyo iliyoendeshwa kupitia Jukwaa la Sanaa ambalo hufanyika kila wiki kiasi cha kuwa dira ya tasnia ya sanaa na burudani, ililenga kuwawezesha wasanii kuendana na wakati.
Kupitia semina hiyo, wasanii walipewa elimu na maeneo ya namna ya kuendeleza wazo hadi sinema ya kusisimua, namna yakufikia hisia za watazamaji, ujenzi mzuri wa matukio, kutengeneza wahusika na mfumo wa hadithi, mwanzo, kati na hitimisho.
Kati ya watoa mada katika programu hiyo maalumu, alikuwa ni Mkurugenzi wa asasi ya Gaba Arts, James Gayo, aliyewataka wasanii kubadilika, kwani umefika wakati kwa wasanii wa filamu kuwa na maarifa zaidi katika kuboresha kazi zao.
Katika hilo, aligusia namna ya kutengeneza sinema zenye visa vipya; zenye weledi na zisizosukumwa na matakwa au maelekezo ya wasambazaji.
Kwamba, kwa vile wenzetu hutamani sana kupata vitu kutoka Afrika vyenye kuzungumzia uhalisia wa maisha ya Mtanzania na Afrika, ni muhimu kuwaonesha vitu vipya katika uandishi wa muswada wa sinema.
Kwamba, suala la uhalisia na visa vyenye utofauti, ni la msingi sana kwani watazamaji wa sinema au filamu, huwa wana kawaida ya kuchoka pale wanapolishwa visa vya aina moja muda wote na akawataka wasanii kujikita kwenye kubuni visa vipya na vyenye kugusa uhalisia wa maisha ya wadau.
Akaongeza kuwa, kama wasanii wetu wa filamu wataendelea kutengeneza kazi zisizo na weledi, zenye visa vilevile na zenye kusukumwa na wasambazaji au haja ya kuchuma fedha za haraka tu, watu watatuchoka na baadaye soko litakufa.
Katika kusisitiza hilo, alitaja sifa za muswada (script) bora kuwa ni kubeba wazo linalozalika kwenye jamii, visa vyenye uhalisia na vipya, utengenezaji mzuri wawahusika na sifa nyingine nyingi.
Naye msanii wa mashairi, Mrisho Mpoto, aliyekuwa kati ya waliohudhuria semina hiyo, alisema wasanii wa filamu wanahitaji kusaidiwa kwani kwa sasa soko la filamu limekuwa la kitumwa na lenye kuburuzwa na matakwa ya wasambazaji bila weledi.
Aidha, Katibu Mtendaji wa BASATA, Ghonche Materego, alishauri wasanii wa filamu kujipanga kushirikiana na wasomi wenye weledi katika maeneo yao ili kuzalisha kazi zenye weledi na ubora.
Materego alitoa ushauri kwa wasanii kuwatumia wataalamu wa fani hiyo kwani licha ya kutingwa na mambo mengi, ni vema wasanii wakawatumia katika kuboresha kazi zao.
Nasi Tanzania Daima tukiwa sehemu ya wadau wa michezo, sanaa, burudani na maendeleo kwa ujumla wake, tunaunga mkono juhudi za Basata na wadau wengine katika kupigania maendeleo ya tasnia hiyo.
Tunaamini kwa dhati kabisa kupitia semina mbalimbali za kitaalamu zinazoendeshwa na Basata kwa ushirikiano wa karibu na wataalamu mbalimbali, sekta hiyo itakuwa yenye masilahi kwa wasanii wetu na taifa.
Tunayasema haya kutokana na juhudi kubwa ambazo zimekuwa zikifanywa na Basata kutoa elimu mbalimbali kwa wasanii wetu namna ya kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi, hivyo kuboresha soko.

Tetemeko La Ardhi Na Mafunzo Tunayopata

Maisha ya dunia sio chochote mbele ya Muumba na yaweza kukatika ghafla bila ya kuletewa taarifa. Tunaamka tukilala tukiwa ni wenye kusindikiza vijana kwa wazee kwenye malazi ya milele ndani ya Barzakh.

Zipo njia nyingi za kukatika maisha haya kama vile ajali, maradhi na mauaji. Hata hivyo, kuna aina nyingine ambayo kwa karne mbili hizi zilizopita, imepamba moto. Ni hii ardhi yetu tunayoringa nayo kushindwa kabisa kuhimili madhambi yetu yaliyopindukia mipaka. Hapo tunaona kimbunga, mitetemeko, kiwango cha juu cha joto au baridi kali na kadhalika.

Ardhi ya China ni mfano mzuri wa kuwazindua ndugu zetu wa Kiislam. Hakika kuna mengi ya kujifunza kwa Waislam kutokana na tetemeko lililotokea tarehe 12 Mei, 2008 huko China.  Maisha ya maelfu yalipotea ghafla bila ya matarajio. Maelfu walipoteza viungo ambavyo kina dada wakivipigia mnada bure kabisa. Maelfu ya matajiri waliokuwa wakitakabbar kwa utajiri, siha na neema aliyowapa Allaah waliondoka kwa wepesi kabisa. Mamilioni ya maisha ya watu yalibadilika ghafla ndani ya kipindi kisichozidi nusu saa... ALLAAHU AKBAR! Yapo wapi macho ya Waislam kutanabahi kiumbe hichi kinachoitwa ardhi kushindwa kuhimili madhambi ya wanaadamu?!

Majanga haya hayajaacha kuganduka kwa China ingawa ina idadi kubwa ya wananchi wake kuwa sio Waislam. Juu ya kwamba wamekuwa na ubinaadamu na moyo wa kusaidia haraka, hata kwa wale waliokuwa hawana uwezo, nao wamejitolea kusaidia. Sisi Waislam leo uwezo tunao, badala ya kusaidiana tunaleta jeuri ya neema tuliopewa.

Ni funzo kwa Waislam kuwa Maneno ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) hayaanguki abadan, kuwa siku za mwisho kutakuwa na majanga mengi, vifo vitatokea vingi kwa pamoja na mengineyo:

{{Uharibifu umedhihiri barani na baharini kwa sababu ya yale iliyofanya mikono ya watu, ili Awaonjeshe (adhabu ya) baadhi ya mambo waliyoyafanya, huenda wakarudi (wakatubia kwa Mwenye Enzi Mungu)}} [Ar-Ruum 30: 41]

Naye Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amekwisha bainisha kuwa maafa yatakuwa ni mengi karibu na Qiyaamah:
“Saa (Qiyaamah) haitosimama hadi elimu ifutwe, wakati kukimbia kwa kasi, mitetemeko kuzidi kwa sana, fitna kutokea na al-Harj kuengezeka.” Ikaulizwa, “Ewe Mjumbe wa Allaah, nini hiyo al-Harj?” Akasema, “Al-Qatl, al-Qatl (mauaji)”. [Imepokewa na Imaam Ahmad]

Na kwa vile maneno ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) pamoja na Mtume Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ni mazima; tujue kuwa mitihani hii ipo, na bila ya shaka kila tuliloahidiwa litatokea, ikiwemo Qiyaamah chenyewe. Kwa mantiki hiyo; tunatakiwa tustaghfiru na tujiweke tayari na kifo wakati wowote.

Hakuna mwenye appointment (miadi) na Malakul-Mawt. Anakuja ule wakati anaopangiwa na Mola wake aje kuzichukua roho zetu. Wachina wale waliokufa kwa mpigo hakuna hata mmoja aliyejuwa kama siku ile angekufa, ya kwamba angekwenda kwa haloo au wakwe zake Japan kwa kukimbia mauti. Laiti ghayb ingejulikana na viumbe, Serikali ya China ingekuwa na uwezo wa kuwahamisha watu wake kutoka kwenye eneo la epicenter kabla maharibiko hayajatokea.

Hili jambo liwaguse wanaosema: "acha nienjoy, mie kijana, bado damu inachemka kotokoto". Waliokufa katika maafa walikuwemo vijana waliochemkwa na damu mpaka zikatokota kwa afya njema na uzuri. Na wale walionekana na maumbo madogo, hawakuwa ni mbilikimo (watu wafupi), bali ni watoto wadogo kuonesha kwamba kifo au maafa hayachagui umri.

Hili jambo pia liwaguse wenye uwezo wanaogoma kuhiji, wakisema kuwa watakwenda baadae. Nadhani, pengine katika mamilioni ya watu wale kuna ambao walikuwa na mawazo kama hayo japo mmoja na hakufanikisha malengo. Na hiyo ni khiyana kwa Allaah mtakatifu tunamfanyia, kuwa Katupa uwezo na tunautumia kinyume na malengo ya Diyn. Liwaguse hili jambo, wale wanaosema watajistiri... tusubiri... tusubiri kwanza...



................................................................



Yawezekana kuwa tafsiri halisi ya neno ndoa imepotea!


Na Abdullrahman Yusuph
NDOA! Ni neno lenye herufi nne tu, lakini tafsiri yake ni kubwa, iliyojitanua katika mawanda mapana na matawi lukuk Ndoa ni taasisi kubwa na ya kwanza, kabla ya zote iliyoanzishwa na Mungu.Katika kitabu cha Mwanzo Sura 2: 24 Biblia inasema:  
“Kwa sababu hiyo mwanaume atamwacha baba yake na mama yake ataungana na mkewe na hawa wawili watakuwa mwili mmoja.”
Mchungaji James Dobson kutoka England anaitafsiri ndoa kama zawadi muhimu ya kudumu wanadamu waliyopewa na Mungu.
Mimi si mtaalamu wa masuala ya uhusiano, lakini yaonekana dhahiri kuwa,  ndoa  siku hizi zimepoteza maana yake.
Ndoa imegeuka na kuwa si wito na kiapo kitakatifu tena, bali imegeuka na kuwa ni mtindo wa maisha.
Maana nzima ya ndoa imebadilika na hapa kila mmoja anakuja na sababu yake ya kuingia katika taasisi hii.
Wengi wanaingia si kwa mapenzi ya kweli, si kwa kuviishi viapo vyao, bali kwa maono yao binafsi tena ya kibinafsi.
Wengine wamekuwa wakifunga ndoa ili wapate zawadi za vyombo katika sherehe za kufundwa au zile za harusi.
Wengine wanakiri kabisa, kuwa, “Niliamua nimuoe kwa sababu alikwishashika mimba.”
Baadhi, huoa au kuolewa kwa sababu tu, “mwenza ana kipato” hivyo anajua hatapata shida ndogo ndogo.
Lakini, tujiulize hii kweli ndiyo maana ya ndoa?
Mwanamke na mwanaume wanaooana, aghalabu hula viapo kuwa watakabiliana na yote yatakayowakuta katika maisha yao. Iwe ni furaha, huzuni, shida, raha, katika ugumba, iwe ni watoto wengi, katika uzee na maradhi.
 Ajabu ni kuwa  viapo hivi huwa  ni vya mdomoni tu na si ajabu kusikia mwanandoa kamtelekeza mwenza wake baada tu ya kuanza kuugua au kufukuzwa kazi.
Sio siri kuwa ndoa zimekuwa nyingi mno siku hizi. Kengele za harusi hugongwa kila kukicha.
Lakini, ukweli ni kwamba, nyingi  zimefunikwa na migogoro …  zikitembea kwa mahadhi ya kutoaminiana, huku  mawimbi ya usaliti yakiwasonga wanandoa. Na mwishowe huvunjika.
Usifikiri ni hadithi, kusikia kuwa bwana harusi alifanya mapenzi na mwanamke mwingine, siku moja kabla ya harusi yake.Si ajabu siku hizi kusikia kuwa, bibi harusi mtarajiwa, kakutwa anafanya biashara ya kuuza mwili viwanja vya Ohio.
Ndiyo maana tunasema ndoa za siku hizi si wito, ni mtindo wa maisha ambao wahusika huujaribu mtindo huo, aidha waonekane nao waliupitia(wasipitwe na wakati) au wanaujaribu kama utawafaa.
Wakati mwingine wanandoa huingia ndoani ili kuwaridhisha wazazi, ambao pengine wanataka mkwe kwa wakati huo.
Maono ya ndoa yanaonekana kuwa yapo mbali mno na wanandoa wenyewe kama zilivyo sayari mbili za Mars na Venus. Wanachokifanya sicho kinachotakiwa ndoani.
Yumkini viongozi wa dini wanashindwa kuwa wakali katika hili au kuweka msisitizo bayana kuhusu kuiheshimu ndoa.
Yawezekana wazazi wameshindwa pia kutilia mkazo umuhimu wa kuithamini taasisi hii.
Lakini kubwa zaidi linaloonekana ni kuwa … hofu ya Mungu haipo.
Woga wa kumsaliti mume au mke umetoweka kabisa. Maana yake ni kuwa, ndoa imegeuka na kuwa si ya watu wawili, lakini yenye matawi kadhaa yasiyo rasmi.
Mchungaji mmoja  aliwahi kuwaasa wanandoa fulani wapya kwa maneno muhimu mno.
Aliwaambia: “Iweni wakarimu kwa watu wote na hasa kwa majirani zenu ili watu wawaombe moto au maji ya kunywa, lakini kamwe msiwe wakarimu katika vitanda vyenu vya ndoa."
Ingawa takwimu rasmi hazijapatikana, lakini idadi ya mabinti waliozaa na waume za watu ni kubwa.
Mabinti hawa, wamekubali kwa radhi ya mioyo yao, kuzaa na waume za watu wakidai kuwa, wataishi maisha huru, tofauti na ndoani.
Swali linaloibuka hapa ni, je, kwa nini wanaume hawa wamezisaliti ndoa zao?
Dini zote duniani hazikubali uzinzi huu, dini ya Kiislamu inaruhusu mke wa pili, lakini kwa kufuata sheria zote.
Wapo pia wake za watu, ambao hudiriki kutembea nje ya ndoa zao.
Upepo huu umewachota hata vjana wadogo ambao tunawaita ‘Kizazi Y’, Ile hofu ya binti au kijana kuwa na uhusiano na mume au mke wa mtu … haipo tena.
Licha ya usaliti wa kutisha katika ndoa, lakini katika nchi  zilizoendelea, siku hizi ndoa ni za kimkataba.
 Kwa mfano, wanandoa wanamuziki, Beyonce na Jay Z, wameoana kwa mkataba. Mkataba huo wa miaka miwili miwili unasema, endapo mwenza mmojawapo atamwacha mwenzake, kabla ya mkataba, basi atamlipa dola milioni kumi.
Je, kuishi kwa mikataba ndiyo maana halisi ya ndoa? Mkataba huu una mapenzi ya kweli au ni  wa kimaslahi zaidi?
Kama wanandoa wanaishi kimkataba, unadhani viapo wanavyokula mbele ya mchungaji, padre  au sheikh ni vya dhati ya mioyo yao?
Baya zaidi ambalo limeibuka miaka ya karibuni ni ndoa za jinsia moja. Wanaharakati wanaozitetea ndoa hizi, wanavitumia vibaya vipengele muhimu kwa wanandoa na kuvihalalisha katika ndoa hizi.
Lakini, vitabu vya dini vinawataja wanandoa kuwa ni ‘Adam na Hawa’ na si Asha na Rose au Juma na Yussuf. Katika taasisi hii ya watu wawili aghalabu tunatarajia matunda ambayo ni watoto yaonekane. Lakini ndoa za jinsia moja  zitaletaje matunda hayo?
Usemi wa ‘ndoa ndoano’ unazidi kupata umaarufu. Hili linatafsiri hasi kwa taasisi hii, inaonyesha kabisa kuwa  imekosa mwelekeo- imelewa kama machela.
Viongozi wa dini wanahitaji kufanya kazi ya ziada ili kuokoa wanandoa. Mafundisho ya kina yatolewe.
Wazazi wawafunde kwa kina wanandoa wachanga, msisitizo uwekwe wakati wa uchaguzi  wa mwenzi.
Lakini ... watu wamwogope kwanza Mungu. Usaliti, ukatili wa kijinsia na zinaa hutokana na kutoweka kwa hofu ya Mungu.
Ndoa inabakia kuwa ni tendo takatifu, tusiigeuze na kuwa chanzo cha vifo-maradhi- uwanja wa mateso na majuto.
 0653-241480

 ..........................................................................................................................

Hasheem Thabeet aja na kliniki ya kikapu June 1-2

Mchezaji wa Tanzania katika ligi ya kikapu ya Marekani, NBA Hasheem Thabeet ‏kwa ushirikiano wa Coca Cola Tanzania kupitia kinywaji cha Sprite ataongoza kliniki ya kikapu kwa vijana itakayofanyika kwa siku mbili nchini.
Kupitia Twitter Hasheem amesema, “Dar es salaam youth basketball clinic coming on your way starting on Thursday  when the kids from all over the country gets here!!!!”
                                                                           Hasheem na famili enzi za utoto wake                                                                 
.

No comments:

Post a Comment

KARIBU