..

..
.

Friday 23 November 2012

DRC:Waasi wa M23 waudhibiti tena mji wa Sake

Waasi wa M23 mjini Goma

Ripoti kutoka DRC zinasema hali ya utulivu imerudi katika mji wa Sake kilomita 27 kusini magharibi mwa mji wa Goma baada ya mapigano kati ya waasi wa M23 na jeshi la serikali likiungwa mkono na wanamgambo wa maimai.
Mji huo unasemekana unadhibitiwa tena na waasi.
Hata hivyo baadhi ya raia wa mji huo wamekimbilia Minova katika mkoa wa Kivu ya kusini na Wengine katika viunga vya mji wa Goma. Mwandishi wetu John Kanyunyu ana taarifa zaidi.
(Kusikiliza taarifa bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini)
 Abdul-Rahman

No comments:

Post a Comment

KARIBU