..

..
.

Thursday 18 October 2012

YANGA YAMALIZANA NA VODACOM JUU YA RANGI YA NEMBO YAO KWENYE JEZI


Kampuni ya simu za mkononi Vodacom, ambao pia ni wadhamini wa ligi kuu ya soka Tanzania bara, wamefikia muafaka na klabu ya Yanga juu ya kutotumia jezi zenye nembo nyekundu.
Vodacom imefikia hatua hiyo kufuatia Yanga kupeleka maombi yao ya kuomba kutotumia nembo hiyo nyekundu katika jezi zao.
Kufuatia maombi ya klabu ya Yanga kupitia kwa viongozi wake na baraza la wazee, vodacom imeona ni busara kuwasikiliza Yanga maombi yao na hivyo kuamua kuipa nafasi ya kuchagua nembo moja kati ya tatu.
Vodacom imetoa aina tatu za nembo na Yanga inapaswa kuchagua moja kati ya hizi nembo tatu.
Swali kwa mashabiki wa Yanga, ipi nembo nzuri kati ya hizi tatu?

No comments:

Post a Comment

KARIBU