Rich Oganiru |
Ni muigizaji maarufu wa filamu hizo na tayari ameshaigiza zaidi ya filamu 300.
Kwa
mujibu wa jarida la National Enquirer la Nigeria, Oganiru anakabiliwa
na kesi nzito ya mauaji ya mke wake mfanyabiashara bilionea aliyekuwa
akiishi Abuja.
Huyo hakuwa mke wake wa kwanza kwani mke wake wa awali naye alikufa katika mazingira yasiyoeleweka miaka kadhaa iliyopita.
National
Enquirer limedai kuwa muigizaji huyo alikuwa akiishi maisha duni kabla
ya kukutana na mwanamke huyo mfanyabishara aliyebadilisha maisha yake.
Inadaiwa
kuwa baada ya kifo cha mke wake aliyezaa naye watoto wawili wa kiume,
alijikuta katika maisha magumu kiasi cha kukosa hata hela kununua
chakula na ndipo alipokutana na mwanamke huyo aliyemwimbisha na
kueleweka hasa kutokana na sura yake kuwa maarufu kwenye filamu.
Ripoti
inasema kuwa baada ya kuishi pamoja na kuoana na mwanamke huyo, Rich
alianza kulalamika baada ya mkewe kushindwa kushika mimba.
Inaendelea
kudai kuwa mke wake alimwamini na kumfanya awe mmiliki wa baadhi ya
mali zake na kuwa mwamuzi wa mambo ya kifedha kwenye kampuni yake.
Baadaye Rich aliingiwa na tamaa na kuanza kuwa na uhusiano na msichana mdogo aitwaye Iyake.
No comments:
Post a Comment