LEMA AJITOSA KUWANIA WAZAZI CCM
Na Benedict Kaguo
VUGUVUGU la uchaguzi ndani ya CCM
limezidi kushika kasi ambapo wanachama wa Chama chicho wameanza mbio za
kuwania nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama hicho kikongwe hapa
nchini.
Uchaguzi huo unatafsiriwa na
wachambuzi wengi wa siasa kuwa ndio dira ya chama hicho kuelekea
uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ambapo CCM na vyama vingine vitasimamisha
wagombea katika uchaguzi huo
Kwa kutambua ukweli juu ya
Demokrasia kubwa iliyoko ndani ya CCM ambayo inampa nafasi kila
mwanachama kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya Chama tayari
wanachama mbalimbali wameshaanza mbio za kugombea nyadhifa mbalimbali
ndani ya chama hicho.
Tayari Mfanyabiashara Maarufu nchini
Bw John Lema ameonesha dhamira ya dhati ya kuwania nafasi ya Mwenyekiti
wa Jumuiya ya Wazazi Taifa ya CCM jumuiya ambayo ndio mlezi wa Chama
hicho kutokana na ukweli kuwa imekuwa mstari wa mbele kuzilea jumuiya
nyingine za Chama hicho.
Bw Lema ambaye mbali na kuwa Mfanyabiashara maarufu pia hadi anawania nafasi hiyo alikuwa ni Mlezi
wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama hicho Mkoa wa Mwanza ambapo kwa kipindi
kirefu amekuwa akikitumikia Chana hicho katika nyanya mbalimbali za
maendeleo ambapo baada ya uzoefu wa kutosha kutoka nafasi mbalimbali
alizokuwa ameshikilia ndicho kilichomsukuma kutangaza kuwania nafasi ya
Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Taifa.
Hata hivyo katika chaguzi mbalimbali
kumekuwepo na masuala ya Rushwa huku baadhi ya wagombea wakionesha
kutumia fedha nyingi kupata madaraka katika eneo hili Bw Lema anamtazamo
gani nalo.
Akizungumza mjini Dodoma Bw Lema
alionya juu ya wagombea wanaotaka madaraka kwa kutumia fedha na kueleza
wazi kuwa hawafai kupewa uongozi kwani pindi watakapopata nafasi hizo
watasahau kukitumikia Chama badala yake wataangalia zaidi kujiineemesha
wao wenyewe.Anasema wanachama
wa CCM wanapaswa kuwaogopa wanaowania uongozi kwa kutumia fedha kwani
wakishapata nafasi hizo watashindwa kuwatumia wananchi,na kwenda
kutafuta maslahi yao binafsi na hivyo kuifanya Jumuiya hiyo kuendelea
kuzorota kimaendeleo licha ya kuwa fursa ya kujiendeleza kichumi.
Anasema
uamuzi wa kugombea nafasi hiyo ya Uenyekiti wa Jumuiya hiyo Taifa
unatokana na rekodi aliyonayo katika kukitumikia Chama hicho tangu ngazi
ya Chikupikizi,Vijana hadi Jumuiya hiyo na kueleza kuwa malengo lukuki
ya kuindeleza Jumuiya hiyo kiuchumi ikiwemo kutumia rasilimali zilizopo .
Anasema Jumuiya hiyo ya Wazazi Taifa
inapaswa kupata viongozi wasiotanguliza maslahi yao badala yake wapewe
nafasi wenye kutanguliza maslahi ya Chama hicho ili kuwezesha mipango
ikiwemo ya kuendeleza rasilimali za jumuiya hiyo kufanikiwa.
Anasema pindi atakapochaguliwa kuwa
Mwenyekiti wa Taifa wa Jumuiya hiyo atasimamia miradi ya Chama hicho
ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imedumaa na kuifanya Jumuiya hiyo kukosa
mapato ya kutosha ya kuendeshea mipango yake.
“Mfano jumuiya ina kiwanja
shekilango Dar es Salaam,tunaweza kujenga hoteli ya nyota tano na kuweka
na kumbi za mikutano itachangia kuleta mapato ndani ya chama na jumuiya
na fedha tunazo kutokana na uzoefu nilionao katika biashara kuweza
kukopa fedha benki kujenga hoteli hiyo,fedha zitatumika kujenga chama na
kurudisha deni la benki… tutaanzisha kitengo cha kulea vijana kwa
kuwatafutia ajira kitakuwa cha vijana wote wa kitanzania hakitaangalia
chama kwa ajili ya kuwatafutia ajira vijana.”alisema Bw Lema.
Kuhusu Sekondari za Jumuiya ya Wazazi CCM
Anasema kilichomsukuma pia kugombea
nafasi hiyo ni hali duni ya Shule za Sekondari za Jumuiya hiyo na kwamba
mkakati wake sasa ni kufufua shule zote za Jumuiya ili ziweze kuendana
na ushindani wa shule zilizopo ziweze kwenda na kiwango bora cha elimu
Anasema kwa muda mrefu Shule hizo
zimekuwa zikitoa elimu duni kutokana na kutokuwepo usimamizi mzuri hivyo
ataimarisha miundombinu ya Shule hizo kuhakikisha zinatoa elimu bora
kulingana na mahitaji ya kitaaluma ya sasa.
Anasema Shule hizo zinapaswa
kuboreshwa ili ziweze kuendana na hali halisi ya sasa na kwamba jukumu
hilo la kuziboresha linawezekana kwa kushirikiana na Wazazi wa Jumuiya
hiyo ili kufanikisha kuwa na walimu bora pamoja na kutoa taaluma
inayokwenda sambamba na mahitaji ya Taifa kwa sasa.
Anasema anachohitaji ni kuungwa mkono na wanachama
wa Chama hicho wakati wa uchaguzi utakapowadia ili kwa pamoja waweze
kushirikiana kuijenga Jumuiya hiyo muhimu hasa katika wakati huu ambao
kumekuwepo na ushindani mkubwa kutoka vyama vya Upinzani.
Hata hivyo jina la
Bw Lema sio jina jipya katika medani za siasa hapa nchini kupitia Chama
cha Mapinduzi kutokana na nafasi mbalimbali ambazo amekuwa nazo ndani ya
Chama hicho ambapo kwa sasa Mlezi jumuiya Wazazi mkoa wa mwanza,
Kuhusu nini kimemsukuma kugombea
Anasema kwa mujibu
wa Katiba ya CCM kila mwanachama ana haki ya kugombea kutokana na
demokrasia,kuleta mabadiliko na mageuzi ndani ya jumuiya wazazi ili
iendane na wakati kiuchumi,iachane kuwa tegemezi ndani ya chama iweze
kujitegemea yenyewe
Anataka Jumuiya
hiyo iweze kuimarika zaidi na kukisaidia chama na kuboresha maslahi ya
watumishi ndani ya jumuiya ili waweze na ari zaidi na nguvu zaidi katika
kuitumikia jumuiya na chama hasa wakati huu ambao kumekuwepo na
changamoto nyingi kutoka vyama vingine vya siasa.
“Mwaka 2008
nilipoteuliwa kuwa mjumbe wa kukusanya fedha za uchaguzi mkuu wa
niligundua mambo mengi ndani ya jumuiya ambayo yako ndani ya uwezo wangu
wa kuweza kuyatatua ili Jumuiya iweze kuwa vizuri kiuchumi”.
“Mfano jumuiya ina
kiwanja shekilango Dar es Salaam,tunaweza kujenga hoteli ya nyota tano
na kuweka na kumbi za mikutano itachangia kuleta mapato ndani ya chama
na jumuiya na fedha tunazo kutokana na uzoefu nilionao katika biashara
kuweza kukopa fedha benki kujenga hoteli hiyo,fedha zitatumika kujenga
chama na kurudisha deni la benki”anasema Bw Lema.
No comments:
Post a Comment