..

..
.

Tuesday 28 August 2012

Kituo cha Vijana wa Kiislamu chaapa kulipiza mauaji ya kiongozi wake Rogo

Mhadhiri wa Kiislamu wa Kenya Aboud Rogo Mohammed, ambaye alikuwa kwenye orodha ya kimataifa ya watu waliowekewa vikwazo kwa kuliunga mkono kundi la al-Shabaab lenye mafungamano na al-Qaeda, alipigwa risasi na kuuawa hapo Jumatatu (tarehe 27 Agosti) akiwa garini mwake mjini Mombasa.
  • Wakenya wamezunguka gari ambayo Rogo Mohammed alipigwa risasi na kufa na watu wenye silaha wasiojulikana huko Mombasa tarehe 27 Agosti [Na Stringer/AFP]
Mashahidi walisema kwamba gari hilo lilitobolewatobolewa kwa risasi. Picha iliyosambazwa na wafuasi wake iliionesha maiti yake ikiwa imerowa damu nyuma ya usukani wa gari.
"Alikufa wakati tukimuwaihisha hospitali," alisema mjane wake, Haniya Said, kwa mujibu wa shirika la habari la AFP kabla ya yeye mwenyewe na watoto wake kupelekewa hospitalini.
Kifo cha Mohammed kilichochea maandamano ya maelfu ya waandamanaji wenye hasira kukusanyika katika msikiti ambao alikuwa akiutumia kutoa hotuba zake mara kwa mara, waliotia moto magari na kupiga mayowe ya kumuunga mkono kiongozi huyo, iliripoti AFP.
"Imamu alipiga kelele kupitia spika ya msikitini "damu kwa damu", na mara moja vijana wakaanza kuyarushia mawe magari," alisema shahidi Dennis Odhiambo, ambaye gari yake iliathirika na akalazimika kukimbilia kituo kimoja cha polisi kwa usalama wake.
Mkuu wa Polisi wa Mkoa huo, Aggrey Adoli, alisema: "Mtu mmoja ameuawa, alikatwa kwa mapanga hadi kufa wakati wa maandamano."
"Kuna vurugu mjini sasa, na maafisa wetu wako huko kuwatawanya waandamanaji kurudisha amani," alisema Adoli.
"Mji mzima uko kwenye hali mbaya, kuna waporaji mitaani, gari zimevunjwa, mengine yamechomwa moto," alisema Francis Auma kutoka Jumuiya ya Waislamu kwa Haki za Binadamu.

No comments:

Post a Comment

KARIBU