..

..
.

Tuesday 10 July 2012

ZIARA YA SIKU MOJA YA MAKAMU WA RAIS WA AFRIKA KUSINI MJINI MOROGORO

MAKAMU WA RAIS WA NCHINI AFRIKA KUSINI,KGALEMA MOTLANTHE ( KATIKATI) AKIANGALIA MOJA YA KABURI LA MPIGANIA UHURU WA ANC , ENEO LA MAZIMBU,MJINI MOROGORO.

Na John Nditi .

Makamu wa Rais wa Afrika ya Kusini, Kgalema Motlanthe, Julai 9, mwaka huu alifanya ziara ya siku moja Mjini Morogoro, ililiyokuwa mahusisi kwa ajili ya kutembelea eneo la Mazimbu, ilikuwa kambi ya wapingania uhuru wa Chama cha ANC.

Ziara hiyo ilikuwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 20 tangu harakati za ukombozi wa Afrika Kusini zilipomalizika ,katika Kambi hiyo , ANC iliacha majengo na vitu mbalimbali vilivyokabishiwa Serikali ya Tanzania, pia yapo makaburi kadhaa walimozikwa mashujaa hao, ambapo Makamu huyo wa Rais aliweza kuzuru na kuweka shada la maua katika mnara wa kumbukumbu ya wapigania uhuru hao pamoja na kupanda mti.

Kabla ya kufanya shughuli hiyo,alipata fursa ya kutembezwa maneo mbalimbali yakiwemo majengo yaliyokuwa yakitumiwa na wapigania uhuru hao, ikiwemo Shule ya Msingi na Awali, Shamba la Mifuko, Kiwanda cha samani pamoja na Hospitali .

No comments:

Post a Comment

KARIBU