..

..
.

Tuesday 12 June 2012

UFARANSA VS ENGLAND: ROY HODGSON NA FALSAFA YA KUPAKI BASI - KAPATA ALICHOTAKA

Hii ilikuwa mechi ambayo ilikuwa na ubunifu mdogo sana huku ikichezwa kwa kasi ya chini sana .
Laureant Blanc aliteua kikosi ambacho kilicheza mfumo ambao kila mmoja alitarajia mfumo wa 4-3-3, huku Florent Malouda akihangaika mbele akitokea katikati ya uwanja.
Roy Hodgson aliwashangaza watu wengi kwa kumpanga Alex Oxlade Chamberlain ambaye alicheza upande wa kushoto huku James Milner akicheza upande wa kulia  na Danny Welbeck akiongoza mashambulizi .
Kama ilivyotarajiwa, Ufaransa ilitawala sana mpira kwa maana ya umiliki huku ikimaliza kwa wastani wa asilimia 65 ya umiliki wa mpira huku wakipiga mashuti 21 tofauti na England ambao walipiga mashuti matano pekee. Hata hivyo mashuti mengi ya Ufaransa yalikuwa ya mbali yasiyokuwa na madhara ukiachilia mbali shuti la Nasri ambalo lilizaa bao la kusawazisha, yote kwa yote Ufaransa walihangaika kutengeneza nafasi za wazi.
Vita ya Mfumo
Ilikuwa vita nyepesi. England walikuwa na makundi ya wachezaji wanne wanne kwenye ulinzi na kiungo huku Ashley Young na Welbeck wakicheza mbele - Laureant Blanc alimpa Alou Diarra maelekezo ya kumkaba Ashley Young na kumnyima nafasi ya kufanya kazi kwa uhuru hasa pale ambapo Young alikuwa anarudi chini kusaka mpira. Yohan Cabaye alikuwa akicheza juu karibu na sehemu aliyokuwa Gerard na Malouda alikuwa akijaribu kumvuta Scott Parker kutoka kwenye nafasi yake aliyokuwa. Kiujumla kulikuwa na nafasi finyu sana kwa Ufaransa kufanya mambo yake kwa uhuru kwani England walijaza upande wao na kuwanyima Ufaransa uhuru wa kupiga pasi walizohitaji kupanga mashambulizi. Ufaransa walijaribu mbinu ya kupitisha mipira jambo ambalo liliwafanya  England kutoa mipira mingi iliyoza kona ambazo hazikuzaa matunda .

No comments:

Post a Comment

KARIBU