..

..
.

Thursday 31 May 2012

Katika kuifanya ligi kuu ya Spain iwe ya ushindani serikali ya nchi hiyo imesema imeanza kuchukua hatua kadhaa moja wapo kuongea na giants wa soka nchini Hispania Real Madrid na Barcelona ambao wanaweza wakawa tayari kushea faida ya haki za matangazo ya Televison miongoni mwa vilabu vya La Liga, kwa mujibu wa Waziri wa Michezo wa nchi hiyo.

Jose Ignacio Wert alisema: "Naamini kwamba Madrid na Barcelona wapo tayari kuweza kushea mapato yatokanayo na kuuza haki za matangazo ya TV.

Vilabu kwenye La Liga huwa vina utaratibu wa kuongea kila mmoja kimpango wake na wamiliki wa TV, tofauti na  ligi nyingine barani ulaya ambazo zina mfumo wa kuungana kwenye suala la haki za  matangazo ya TV. Real na Barca wanapata nusu ya mapato yote yatokanayo na kuuza haki za matangazo ya mechi - nusu ya £511million.

Utafiti uliotoka mwezi April na chuo kikuu cha Barcelona, ulionyesha kwamba kwenye msimu wa 2010-11 Barca walipata kiasi cha £130 kutokana na haki za matangazo ya TV, Madrid walipata £124million huku Valencia wakipata £33.5million.

No comments:

Post a Comment

KARIBU