..

..
.

Thursday 31 May 2012

IKER CASILLAS AMFIKIA EDWIN VAN DER SAR KWA CLEAN SHEETS ZA MECHI KIMATAIFA

Golikipa wa timu ya taifa ya Spain Iker Casillas amefikia rekodi mbili kubwa katika mechi za kirafiki hivi karibuni.

Katika mechi ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Serbia wikiendi iliyopita ilikuwa mechi ya 73 kwa golikipa wa Real Madrid kutoruhusu wavu wake kuguswa katika mechi 130 za kimataifa - na kumfanya kuipita rekodi ya zamani iliyokuwa imewekwa na golikipa wa zamani wa Uholanzi Edwin van der Sar.

Ushindi wa siku ya jumatano ya juzi dhidi South Korea, kwenye mechi ambayo Casillas aliingia kama mbadala wa Pepe Reina, ulikuwa ushindi wa 95 kwa Caillas kwenye 130 alizoichezea Spain. Hilo lilimfanya awapite mlinzi wa zamani wa Ufaransa Lilian Thuram na babu wa Misri Ahmed Hassan.

Ahmed Hassan anashikilia rekodi ya kucheza mechi nyingi za kimataifa, akiichezea Misri mechi 181. Ikiwa Casillas atakuwa safi kiafya na uwezo wake ukiendelea kuwa juu basii inatabiriwa kuwa mpaka 2017 ambapo atakuwa na miaka 36 atakuwa amemfikia Ahmed.

No comments:

Post a Comment

KARIBU