..

..
.

Saturday 20 July 2013

Bomu la barabarani lapiga msafara wa AMISOM, waandishi 2 wapigwa risasi

Milipuko ya kando ya barabara iliyoulenga msafara wa Kikosi cha Umoja wa Afrika cha Kulinda Amani nchini Somalia (AMISOM) baina ya Kismayu na makutano ya Afmadow iliwajeruhi wanajeshi watatu na raia wawili siku ya Jumatano (tarehe 17 Julai), ilisema AMISOM kwenye taarifa yake kwa vyombo vya habari.
"Tunalaani vikali mashambulizi ya woga ambayo yamehatarisha maisha ya watu wa Kismayu," alisema Kamanda wa AMISOM, Luteni Jenerali Andrew Gutti. "Mashambulizi haya hayatazirudisha nyuma juhudi zetu za kuwalinda na kuwasaidia watu wa Somalia katika wakati wakiijenga nchi yao."
Waandishi wawili wa habari waliokwenda kuripoti tukio hilo walipigwa risasi na watu wenye silaha wasiojulikana, liliripoti shirika la habari la AFP.
Mascud Abdulahi Adan, ripota wa Redio Dalsan, alijeruhiwa vibaya kwa risasi ya shingo, ambapo Mohamed Farah Sahal, anayefanya kazi na Redio Goobjoog, alipigwa risasi begani, kwa mujibu wa Chama cha Waandishi wa Habari cha Somalia.
"Mascud alikuwa akijaribu kuripoti mashambulizi hayo ... na alikuwa njiani kwenda kwenye tukio pale alipopigwa risasi, alisema mkurugenzi wa Redio Dalsan, Hassan Ali Gesey.
Haikuwa wazi ikiwa waandishi hao walilengwa wao moja kwa moja.

No comments:

Post a Comment

KARIBU