..

..
.

Monday 19 November 2012

Tanzania kuweka kumbukumbu kuu kwa wafanyakazi wa kigeni

Serikali ya Tanzania inapanga kuhakiki wafanyakazi wa kigeni walioajiriwa katika sekta binafsi, Waziri wa Kazi na Ajira Gaudensia Kabaka alitangaza mjini Dar es Salaam siku ya Ijumaa (tarehe 16 Novemba).
Kwa sasa serikali haina data kwa kina zinazowahusu wageni wanaofanyakazi nchini, na kuifanya hali hiyo kuwa changamoto katika kutekeleza sera zilizobuniwa kwa ajili ya kuongeza ajira kwa Watanzania, Kabaka alisema, kwa mujibu wa gazeti la The Guardian la Tanzania. Vibali vya mtu mmoja mmoja vinatolewa kwa wageni, lakini serikali haiweki kumbukumbu moja kuu kwa vibali kama hivyo.
Akizungumza katika mkutano wa mwaka wa Jumuiya ya Waajiri Tanzania, Kabaka aliwahimiza waajiri wawe tayari kutoa taarifa za waajiriwa wao ili zoezi hilo lifanyike katika sekta zote. Kuanzia mwezi ujao, serikali itasambaza fomu za uchunguzi kila mwezi kwa waajiri ili kuelezea jinsia, mishahara na aina ya kazi za waajiriwa wao.
Ukosefu wa ajira kwa vijana hasa unahitaji kushughulikiwa na serikali, Kabaka alisema, pamoja na mishahara duni ambayo haikidhi mahitaji kwa viwango vya maisha vinavyotosheleza. Sekta binafsi inaajiri karibu ya asilimia 97 ya nguvu kazi ya nchi, alisema.

No comments:

Post a Comment

KARIBU