..

..
.

Friday 31 August 2012

JIPYA LILILOSEMWA NA CHAMA CHA WALIMU KUHUSU SERIKALI NDIO HILI.

                     Hii ilikua wakati wa mgomo wa walimu uliopita.
Chama cha walimu (CWT) kimesema pamoja na bunge la Jamuhuri ya muungano wa Tanzania na Mahakama kuagiza chama hicho na serikali kurudi kwenye meza ya mazungumzo kwa lengo la kuyapatia ufumbuzi madai ya walimu, bado serikali haijaonyesha utayari wowote wa kufanya hivyo.
Rais wa CWT Gratian Mukoba amesema chama kimechukua hatua mbalimbali ikiwemo kumwandikia barua katibu mkuu kiongozi zaidi ya mara moja kuonyesha utayari wa CWT kukutana na Serikali kwa majadiliano lakini hadi sasa hakuna taarifa yoyote kutoka serikalini.
Amesema kitendo cha serikali kukaa kimya kwa muda wa siku 27 bila kuonyesha kujali kutekelezwa kwa amri ya Mahakama, kinatafsiriwa na CWT kama ni kukosekana kwa nia njema ya serikali kusikiliza madai ya walimu.
Kwenye line nyingine, CWT kimeitaka serikali kuwaachia huru baadhi ya viongozi wa CWT na walimu wote waliofunguliwa mashtaka ikiwa ni pamoja na kuwarejeshea madaraka walimu 15 waliovuliwa vyeo vyao kutokana na mgomo wa walimu.

No comments:

Post a Comment

KARIBU