..

..
.

Tuesday 17 July 2012

Tanesco yaendelea na Zoezi lake la Kukamata wanaoiba Umeme jijini Dar

Meneja wa Tanesco kanda ya Temeke,Richard Mallamia akiwaonyesha waandsishi wa habari mita iliyochezewa na kuunganishwa umeme kinyume na mfumo wa kawaida ilikuiba umeme kwenye duka moja eneo la Kigamboni ambapo zoezi la kukamata wezi wa umeme linaendelea.
Mafundi wa Tanesco wakipitia pita iliyokuwa ikitumika kwa kuiba Umeme.
Mfanyabishara duka na migahawa ya eneo la Kigamboni Jamal Hassan, akipanda kwenye gari la Tanesco kanda ya Temeke ili kumpeleka kwenye kituo cha polisi kutoa maelezo ya kwanini anaiba umeme.

Picha/Habari na Said Powa wa Globu ya Jamii.

SHIRIKA la Umeme Tanesco kupitia kanda zake maalum za Ilala na Temeke jana limeendelea na operesheni zake za kukamata wezi wa umeme wanaochezea mita na wanaojiunganishia bila ya utaratibu maalum.

Wakizungumza kwenye operesheni hiyo kwanyakati tofauti Mameneja hao walieleza namna operesheni hizo zinavyosaiia kuwakamata wahalifi wa mita za umeme na kumekuwa na ufanisi mkubwa tangu kuanza kwa zoezi hilo.

Meneja wa kanda ya Ilala Mhandisi Athanasius Nangalia, mesema tangu zoezi hilo limeanza mwezi mmoja uliopita wamefanikiwa kukagua wateja 4700 na kufanikiwa kukamata wezi wa umeme 51 ambao kutokana na faini walizo lipa wamefanikiwa kukusanya shilingi 45 Millioni.

Aidha Nangali alifafanua kua pamoja na ukusdanyaji huo pia waligundua watu wanaojiunganishia umeme bila ya utaratibu kwa kujiwekea nguzo zao wenyewe lakini wamedhibiti vitendo hivyo kwa kukamata nguzo 18 kwenye maeneo mbalimbali ya Ilala.

Aidha kwenye zoezi lililoendelea jana eneo la Upanga liliambatana na vituko kutoka kwa wenye nyumba baada ya kujifungia ndani na kukataa wakaguzi hao wasiingie ndani ya nyumba hizo hata hivyo waliamua kubandika ujumbe kwenye mageti hayo unaoeleza namba za mwisho za mita zilizo somwa na zilizopo sasa.

KWA UANDE WA Temeke zoezi hilo limefanyika eneo la kigamboni na kufanikisha kutiwa mbaroni kwa watu watatu ambao wanatuhumiwa kujihusisha na wizi wa umeme.
 

No comments:

Post a Comment

KARIBU