..

..
.

Saturday 7 July 2012

Jason Derulo kutua rwanda

Imethibitika kwamba staa wa ngoma ya Watcha Say, iliyotoka mwaka 2009, na kuvuma mwaka jana hapa nchini, jason derulo ndio atakuwa mtumbuizaji mkubwa kwenye fainali za  shindano kubwa la muziki nchini Rwanda, lijulikanalo kwa jina la Primus Guma Guma Superstar ambalo linafanyika kwa mara ya pili nchini humo.Habari za uhakika zinasema kwamba Derulo kwa kushirikiana na wasanii wakubwa wa rwanda, watapanda jukwaa moja tarehe 29 ya mwezi huu, huku yeye akiwa kama mtumbuizaji, na wasanii wa Rwanda wakichuana ili kumpata staa mkubwa wa ukweli kutoka nchini humo, miongoni mwa wale wanaowika.Mwaka jana, shindano hilo lilifanyika na mwanamuziki wa R&B nchini humo Tom Close, aliibuka mshindi.Tofauti ya shindano hili na mashindano kama BSS na Tusker Project Fame, ni kwamba lenyewe hushindanisha wasanii waliofanikiwa tayari  na wasanii kumi pekee ndio huchaguliwa kushiriki, kama ilivyokuwa kwa Mfalme wa Rhymes Tanzania.Wasanii hao hutumia nyimbo zao wenyewe wakati wa shindano hilo.Vigezo vya wanamuziki kushindana kwenye shindano hilo ni lazima awe na miaka 18 na kuendelea, awe na wimbo uliohit na awe anafanyia muziki nchini Rwanda.

No comments:

Post a Comment

KARIBU