..

..
.

Thursday 21 June 2012

MAAJABU: WANAIJERIA HUUZA FIGO KWA SH MILION 51($30,000)

Baadhi ya wanaijeria waishio nje ya nchi wamejikuta wakiwa na maisha magumu kiasi cha kuamua kuuza figo zao ili waweze kuishi.
Biashara hiyo iliyoshamiri kwenye mtandao imewafanya baadhi yao kutafuta soko la viungo hivyo muhimu kwenye mwili wa binadamu na wengine wakisafiri hadi Malaysia na India kuuza figo zao zote mbili kwa $30,000.
Kwa mujibu wa mtandao wa nigeriafilms.com, watafiti wake wamebaini kuwa kuna mtandao mkubwa sana wa wafanyabiashara, mawakala, wauzaji wa watafutaji wa bidhaa hiyo ambao hutafuta watu watakaouza figo zao.Wengine hufikia hatua za kuteka watu na kuwanyofoa figo zao ili kujipatia maisha mazuri na ya haraka.Kuna taarifa kuwa watu wengine hupoteza maisha wakati wa oparesheni ya kunyofoa figo hizo.Mpaka sasa karibu wanaijeria 1000 wana matumaini ya kupata connection hizo ili nao waweze kuuza figo zao na kujipatia maisha wanayoyataka.Mtandao huo umemaliza kwa kusema, “Hivi ndivyo umaskini unaosababishwa na uongozi mbovu umeifikisha Nigeria.”

1 comment:

  1. Hayo ni maisha magumuau maamuzi kweli mtu mwenye akili yake hufanya hivyo kali ya mwaka

    ReplyDelete

KARIBU