..

..
.

Thursday 14 June 2012

 Katibu Mkuu wa Umoja wa  Mataifa, Ban Ki Moon akiwa na Dkt Asha-Rose Migiro katika hafla ya kumuaga rasmi iliyofanyika leo katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa baada ya kumaliza muda wake kama Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa


Mashirika ya  Umoja wa Mataifa yanayohusika na  masuala ya  Idadi ya Watu 
( UNFPA),Ugonjwa wa Ukimwi ( UNAIDS) na   Mpango wa  kupambana na Ugonjwa wa Malaria ( RBM) jana jumanne yaliandaa tafrija kamambe ya kumshukuru  na kumuaga Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dkt. Asha-Rose Migiro.
 
 Tafrija hiyo ya aina yake  na ambayo  mgeni  rasmi alikuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa  Mataifa, Ban Ki Moon,  akiambatana na mke wake na kuhudhuriwa pia na  wadau  mbalimbali  akiwamo Mtendaji  Mkuu wa UNDP Bi Helen Clark, mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao katika UM,  sekta binafsi na taasisi za kiraia imefanyika hapa makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.
 
Akizungumza wakati wa  tafrija hiyo, Katibu Mkuu Ban ki Moom ameleezea baadhi ya  sababu  zilizomsukuma  kumteua Dkt. Asha- Rose Migiro kuwa msaidizi wake wa karibu.
 “ Nilianza kumfahamu Asha- Rose Migiro wakati huo sote tukiwa mawaziri wa mambo ya nje  katika nchi zote. Uwezo wake na uelewa wake wa mambo ulinivutia sana, lakini nilivutiwa zaidi pale nilipofahamu kwamba aliwahi kuwa waziri anayehusika na masuala ya wanawake na watoto. Nikajiridhisha kwamba huyu ndiye alikuwa ananifaa kuwa msaidizi wangu wa karibu” akasema Ban Ki Moon na kuufanya umati ulihohudhiria tafrija hiyo kushangilia kwa nguvu.
 
 Kama hiyo haitoshi, Ban Ki Moon amemuelezea Dkt. Asha- Rose Migiro kama msaidizi wake wa karibu ambaye licha ya kufanya kazi kwa uadilifu mkubwa lakini ni mtu ambaye alikuwa hana makuu na wala hata siku moja hakujikweza.
“ Katika kipindi chote ambacho Migiro amekuwa msaidi wangu wa karibu, amenisaidia katika mambo mengi, ni mtu muadilifu sana, ni mtu aliyekaribu sana na watu, aliyeamsha matumaini na kuwapa tabasamu watu waliokuwa katika mazingira magumu.  Daima amekuwa mstari  wa mbele kunisaidia  na hakuna hata siku moja alipojikwenza. Na kwa sababu hii  anastahili tafrija hii” akasisitiza Ban Ki Moon.
Aidha Ban Ki Moon akamuelezea  Asha- Rose Migiro kama kiongozi ambaye daima alitoa kipaumbele  cha aina yake katika masuala ya afya ya jamii  eneo alilotumia uwezo wake wote, maarifa yake yote kama naibu katibu mkuu kupigania afya ya wanawake na watoto na watu wote walio katika mazingira magumu

No comments:

Post a Comment

KARIBU