..

..
.

Sunday 27 May 2012

Riadha Kenya (AK), chombo kinachoshughulika na riadha nchini, kinapanga kuandaa mfululizo wa mashindano ya mbio ndefu mapema mwaka ujao ili kuibua vipaji vilivyojificha katika Mkoa wa Kaskazini Mashariki.
  • Mkimbiaji wa Kiingereza mwenye asili ya Somalia Mo Farah akiongoza katika mbio za maili mbili kwenye mashindano ya Aviva Grand Prix Birmingham hapo Februari. Maafisa wa Mkoa wa Kaskazini Mashariki wanatarajia kuwa Farah atawatia moyo wanariadha katika eneo hilo. [Na Abdullrahman yusuph wa Tanga ]
Mwenyekiti wa AK Isaiah Kiplagat alisema hii ni mara ya kwanza kwa tukio kubwa la riadha kama hili kuanzishwa mkoani. Alisema AK inataka kuinua mwamko wa riadha katika mkoa na inatumai kuwa baadhi ya wanariadha wa juu watakuja kukuza mchezo huo.
Ili kuusaidia mkoa kufikia uwezo wake kamili, AK imewapa mafunzo makocha 15, Kiplagat alisema.
“Tumekuwa tukituma timu za Kenya katika mashindano ya kimataifa, lakini inavunja moyo kuwa mwaka baada ya mwaka, hakuna yeyote kutoka mkoa huu anayeshiriki – hata katika mashindano ya kitaifa,” aliiambia Sabahi

1 comment:

  1. kweli si mchwzo kila kitu kuamua na mazoezi hawa jamaa wanaweza kukimbia karibia nusu nchi

    ReplyDelete

KARIBU