..

..
.

Tuesday 29 May 2012

MTATIRO: HILI LA ZANZIBAR HALIUNGWI MKONO “LABDA NA MWENDA WAZIMU TU”


JULIUS MTATIRO katibu mkuu wa chama CUF Tanazania bara
*********************
Habari za uchomaji wa makanisa Zanzibar katika vurugu za hivi karibuni haziungwi mkono kwa namna yoyote ile. Yeyote anayefanya vitendo hivi ni gaidi kwa sababu anafanya vitendo vya kigaidi. Serikali ya zanzibar ichukue hatua kali sana za kisheria kwa yeyote aliyehusika na vitendo hivi bila kujali yeye ni nani.

Kuchoma makanisa ni jambo la hatari sana, sielewi anayefanya hivi yeye ni dini gani, sijui ni dini ipi inayoruhusu uchomaji wa nyumba za ibada za dini nyingine, ni dini ya shetani peke yake inaweza kufanya hivyo.

Kuna watu wanasema ati ni “waislamu” ndiyo wanafanya vitendo hivyo, mie nakataa, nasema wanaofanya hivyo siyo waislamu.

 Waislamu walioko Zanzibar naowajua mimi ni wakarimu, ni watulivu na wasikivu na wanapenda amani. Hata mapambano ya wafuasi wa CUF na CCM yaliisha kwa wao wenyewe kuridhiana.
Wazanzibari siyo wakatili kiasi hiki. Kuchoma makanisa hakuwezi kufananishwa na kuchoma Mahakama, ikulu,polisi n.k. Uchomaji wa makanisa au misikiti ni uchonganishi mkubwa unaoibua vita mahali pengi duniani. Anayefanya hivyo ana malengo mabaya sana siyo kwa wananchi wa Zanzibar tu bali kwa wananchi wa wa Tanzania kwa ujumla.

Hii ni kwa sababu makanisa yakishachomwa tetesi zinasema wamechoma waislamu(jambo ambalo siliamini), tetesi hizi zikizidi na pakatokea athari kubwa kwa makanisa na labda watu(wakristo) wakachomwa na kufariki ndani ya makanisa hayo, ina maana wakristo watapoteza ndugu zao.

No comments:

Post a Comment

KARIBU