..

..
.

Saturday 24 August 2013

Mechi ya leo JKT Oljoro Vs Coastal Union katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

 
 Mwenyekiti wa Coastal Union Hemed Hilal 'Aurora' akisalimiana na Yayo Kato, kabla ya mpira kuanza.

                                         Kikosi cha leo hiki kilichoanza dhidi ya Oljoro JKT.




                         Yayo Kato akituliza mpira mbele ya Majaliwa Mbaga wa JKT Oljoro.

 Mashabiki wa Coastal Union waliuteka uwanja wa Sheikh Amri Abeid leo. Watu wote mazungumzo ni kigoma hiki.

 Yusuf Machogote wa JKT Oljoro akijaribu kukimbilia mpira na Suleiman Selembe leo.

 Hiki ni kipindi cha pili Selembe alikosa bao la wazi yeye na golikipa. Na hili lilikuwa bao la pili kukosa baada ya kipindi cha kwanza kupewa pasi murua na Yayo akabaki na golikipa akapiga kichwa mpira ukatoka nje.

 Uhuru Suleiman akijaribu kutafuta mbinu za kumtoka mchezaji wa Oljoro leo.

 Selembe akimpongeza Abdi Banda baada ya kufunga bao la kwanza ndani ya dakika 16 ya mchezo.

 Hapa Banda akiwa anarudi kutoka kufurahia na mashabiki wa Coastal Union waliofurika uwanjani leo.

 Mwamuzi wa leo kutoka Mwanza Jacob Adengo akimwonyesha kadi ya Njano Banda kwa kutoka nje ya uwanja wakati mpira ukiendelea.

 Shaaban Kado leo alikuwa nyota ya mchezo baada ya kuopoa michomo mingi ambayo iliyawacha watu mdomo wazi.

 Hapa mashabiki wa Oljoro wakiingia uwanjani kipindi cha pili baada ya kupigiwa simu waje kuongeza nguvu maana kigoma cha Wagosi kiliwazidi nguvu.

                                                 Morocco akisisitiza jambo uwanjani.

                                                         Doctoooor au basi......

               Haruna Moshi Boban leo alivutia watu wengi kutokana na style yake ya kucheza.

 Hamad 'Basmat' akikokota mpira bila wasiwasi wowote, leo alipiga beki nzuri hakuna mchezji aliyethubutu kumsogelea.

                                                Selembe akituliza mpira kwa ufundi mkubwa.

                         Haruna Moshi 'Boban' akituliza mpira mbele ya wachezaji wawili wa Oljoro.


              Mashabiki wa Coastal Union baada ya mpira kuisha ilikuwa raha tu mwanzo mwisho.

Nassor Binslum, Akida Machai na Heme Hilal wakiwa katika viunga vya jiji la Arusha baada ya mechi kuisha kwa ushindi 2-0.

No comments:

Post a Comment

KARIBU